ANGALIA LIVE NEWS

Friday, March 21, 2014

MCHAWI AKAMATWA USIKU WA KUAMKIA LEO KANISANI

Angalia picha za mtu aliyejitambulisha kwa jina la Shabani Hamisi alikuwa akijihusisha na vitendo vya kishirikina, akiwa chini ya wanamaombi wa kanisa la Ufufuo na Uzima Arusha mara baada ya mtu huyo kukamatwa usiku wa kuamkia leo wakati wa maombi kanisani hapo ambapo ametoa maelezo mbalimbali namna alivyokuwa akishiriki katika vitendo hivyo vya kishirikina.
Shabani akiwa na vitenda kazi vyake akiwa eneo la kanisa.
Akiwa amevua shati huku akiwa anaombewa.
Vitenda kazi vyake vikiwa vimemwagwa chini.

Kazi kwelikweli.
Alikosea njia meeen, akakutana na Yesu meen. Picha kwa hisani ya Ufufuo Crew.
Katika hali isiyo ya kawaida mtu huyu ajulikanaye kwa jina la Shabani Hamis amenaswa akiwa anafanya uchawi katika kanisa la Ufufuo na Uzima Arusha.

Matukio ya kunaswa wachawi yamekuwa mengi kanisani hapo kutokana na uweza wa Mungu unaojidhihirisha kupitia Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo, Frank Andrew.

Pamoja, na kukutwa bila nguo mtu huyo aliyekuwa amebeba vifaa ambavyo kwa mujibu wa maelezo yake, huvitumia kuwanga na kupaa ni pamoja na tunguli na kikapo cha mkoba wa uchawi. Tukio hilo la aina yake limetokea Usiku wa saa sita, wakati mkesha wa maombi ukiendelea kanisani hapo.

Baada ya maombi makali ya kuharibu uchawi katika anga la Arusha, ikafuatiwa na tukio hilo. Mungu ni mkuuu maana hapana uchawi wala Uganga juu ya watu wa Mungu.

Information Ministry - Arusha

2 comments:

Anonymous said...

Sad,does this man have any rights? Can he be represented by a lawyer to safegurd his dignity? these things of finding witches in Churches started in Nigeria and what happened next - they accused children as young as 2 months for bringing witchcraft to families.They killed children or kicked them out of homes. I suspect some churches need this to gain acceptance among believers. Can people just go to church to thank God and pray for good health and God's grace as it used to be in traditional churches? No witches, no bringing back the dead, no miracles just prayers and meeting friends and families. What happened? I am not Christian but I used to go to Church for Weddings, Easter, Baptism etc. I have family and friends and they encouraged me to go with them. My knowledge of Church was a friendly place, a place of acceptance and meditation. Place of unity and love. Not accusing anyone. The accusations was left to Courts and Mabaraza husika. God help us all

Anonymous said...

tunaomba ufafanuzi kidogo huyo kijana ni mwendawazimu anakaa kijenge ya chini...imekuaje akawa mchawi tunaomba waandishi mufuatilie zaidi mtupe ufumbuzi juu ya huyo kijana