Advertisements

Monday, April 14, 2014

Diamond na Wema kufunga ndoa mwezi August.

Famous celebrity couple inayo-hit sana hapa town, Wema Sepetu na Diamond Platnumz kutarajia kufunga ndoa na kuwa mume na mke mwishoni mwa mwaka huu, hii ni kutokana na mtabiri maarufu kutoka nchini Tanzania.
blogger-image-788526582
Yahya Hussein ni mtabiri maarufu mwenye makazi yake jijini Dar es salaam na amefanikiwa kutabiri mambo mengi sana kuhusu wapendanao hao, Yahya Hussein anatabiri kuwa ifikapo mwezi wa nane mwaka huu,wawili hao watakuwa mume na
mke,aliongezea nakusema kuwa inabidi wahakikishe harusi hiyo inafanyika la sivyo, itawabidi wasubiri hadi mwaka 2016 tena mwezi wa nane.
“Ndoa yao inabidi ifanyike katika mwaka unaogawanyika kwa mbili” alisema Hussein.
1011606_824750090872818_1610966289_n
Diamond Platnum na Wema Sepetu wameweza kupitia mengi sana katika maisha yao ya mahusiano, hadi kufikia kuachana na baadae, walirudiana mapema baada ya Diamond kuachana na celebrity mwingine maarufu kama Dvj Penny, mtabiri huyo anatabiri kuwa vikwazo vengi vitazidi kutokea katika mahusiano yao, nakuwashauri kuvumilia hayo yote yajayo na kukaa pamoja waweze kuyapita yote hayo.
 vibe

1 comment:

Anonymous said...

Hizi ndoa za kuelezewa na waganga wa kienyeji,mbona wahusika hawajatamka lolote.