ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, May 8, 2014

JUMUIYA YA WATANZANIA DMV

             TANGAZO MAALUM:
Kamati ya Uchaguzi wa viongozi wa jumuia ya Watanzania DMV imeanza kuandaa utaratibu na mchakato wa kuwachagua viongozi wetu.  Watanzania sote tunahamasishwa tushiriki kwa umoja katika zoezi hili adhimu ili tupate viongozi bora  watakaotusogeza mbele  kijamii na kibinafsi.
Kamati hii inawatambua Watanzania  na marafiki zao wote kwa mujibu wa katiba. Wanajumuia hao kwa pamoja ni:
1)   Wale  raia waliolipia ada kamili;
2)   Wale   wasio raia wenye mnasaba na  wale waliolipia ada kamili; na
3)   Wale raia ambao hawakulipia ada lakini kwa njia moja au nyingine anajuhusisha na jumuia.

Ni dhamira ya Kamati kwa mujibu  wa katiba kuwatambua hao wanajumuia kwa kadiri ya ushiriki wao, na hivyo mchakato wa kupiga kura  utatambua michango ya kila  mpiga kura.

Ratiba kamili ya  utaratibu na maagizo mengine kuhusu ugombeaji wa cheo utafuata punde.

No comments: