ANGALIA LIVE NEWS

Friday, May 9, 2014

JUMUIYA YA WATANZANIA DMV

TANGAZO MAALUM:
Kamati ya Uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya ya Watanzania DMV imeundwa na imeanza kuandaa utaratibu na mchakato wa kuwachagua viongozi wetu.  Watanzania wote tunahamasishwa tushiriki kwa umoja katika zoezi hili adhimu ili tupate viongozi bora watakao tusogeza mbele kijamii na kibinafsi.
Kamati hii inawatambua Watanzania  na marafiki zao wote kwa mujibu wa katiba. Wanajumuiya hao kwa pamoja ni:
1)   Wale raia waliolipia ada kamili;
2)   Wale wasio raia wenye mnasaba na  wale waliolipia ada kamili; na
3)   Wale raia ambao hawakulipia ada lakini kwa njia moja au nyingine wanajihusisha na Jumuiya.

Ni dhamira ya Kamati kwa mujibu wa katiba kuwatambua hao wanajumuiya kwa kadiri ya ushiriki wao, na hivyo mchakato wa kupiga kura  utatambua michango ya kila  mpiga kura.

Ratiba kamili ya utaratibu na maagizo mengine kuhusu ugombeaji wa cheo utafuata punde.

3 comments:

Anonymous said...

".............. 3)Wale raia ambao hawakulipia ada lakini kwa njia moja au nyingine wanajihusisha na Jumuiya.

Ni dhamira ya Kamati kwa mujibu wa katiba kuwatambua hao wanajumuiya kwa kadiri ya ushiriki wao, na hivyo mchakato wa kupiga kura utatambua michango ya kila mpiga kura."

Swali: Hivi Katiba ya Jumuiya ndiyo imetoa "Blank Check" kama hii kwa Kamati ya Uchaguzi?

Anonymous said...

Asanteni wana DMV. Tunaoba mtujulishe tulipeje au kwa nani hizi ada jamani wengine inatupa shida kuzilipa account ipi hiyo??
Asante

Anonymous said...

Wasiliana na viongozi wa DMV, ina maana wewe hujui mawasiliano ya viongozi wako?
Go to this website ina maelezo yote ya kufanya malipo na namba za simu za viongozi wako.

http://watanzaniadmv.org/membership.html