Friday, May 30, 2014

NAPATA WAKATI MGUMU SANA KUTAARIFA KIFO CHA MLINZI WA AMANI-BAN KI MOON

 Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akipokea  kutoka kwa Mkuu wa  Idara ya Operesheni za Ulinzi wa  Amani, Bw. Herve Ladsous   Medali ya  Dag Hammarskjold kwa niaba ya mashujaa 10 watanzania waliopoteza maisha mwaka jana huko Darfur na DRC.  Nyuma  ya Balozi ni Lt  Kanali Wilbert Ibunge, Mwambata Jeshi Uwakilishi wa Kudumu.
 Sehemu ya wageni waliohudhuria  hafla  hiyo ambayo awali ilitanguliwa na uwekaji wa Shada la Maua kwa  heshima ya mashujaa hao
 Hii ndiyo Medali wanayopewa walinzi wa amani ambao wamepoteza maisha wakitekeleza jukumu lao la  kulinda amani, Medali hii hupewa Familia ya Marehemu si ya kuvaa bali ni ya kuweka nyumbani
 Bango lenye Majina ya Walinzi wa Amani 106 ambao wamepoteza maisha  mwaka 2013 wakati wakitekeleza dhamana ya  ulinzi wa Amani chini ya Mwamvuli wa Umoja wa Mataifa.  Kati ya walinzi hao 106 wamo watanzania 10
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban Ki Moon, akizungumza wakati wa hafla ya siku ya Kimataifa ya  kuwakumbuka na kuwaenzi walinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa, pamoja na  106 waliopoteza maisha mwaka jana, kumbukumbu hiyo hufanyika  Mei 29 kila mwaka.  Katika Salamu zake, Katibu Mkuu ameeleza kwamba hupata wakati mgumu sana kumtaarifu  Mwakilishi wa Kudumu wa nchi ambayo  Mlinzi wake wa Amani au Walinzi wake wa Amani wamepoteza maisha wakati wakitekeleza majukumu yao.
Balozi Mwinyi akisaini kitabu  na nyuma ni Lt Kanali Wilbert Ibunge

No comments: