Wabunge wanaowakilisha chama kipya cha kupigania haki za kiuchumi za Waafrika Kusini
(Economic Freedom Fighters EFF) leo walizua kihoja baada kuingia bungeni wakiwa wamevalia kama wafanyikazi wajakazi na wachimba migodi .
(Economic Freedom Fighters EFF) leo walizua kihoja baada kuingia bungeni wakiwa wamevalia kama wafanyikazi wajakazi na wachimba migodi .
Wabunge wanawake walivalia sare za mayaya na
wahudumu wa
nyumbani huku wabunge wanaume wakivalia magwanda kama yale
yanayotumika migodini na wafanyikazi wanakandarasi.
EFF
inayoongozwa na aliyekuwa kiongozi wa kitengo cha vijana katika ANC
Julius Malema ilishinda viti katika maeneo bunge 25 katika bunge hilo
lenye uwakilishi bunge 400 katika uchaguzi uliofanywa majuzi.
Malema aliyeunda chama hicho baada ya kutimuliwa kutoka kwenye ANC mwaka wa 2012
Malema aliibua hisia miongoni mwa mamilioni ya
wapiga kura Waafrika weusi aliposema kuwa atapeleka miswada bungeni kwa
lengo la kutaifisha mashamba ya wazungu wachache ilikupunguza mzigo wa
umasikini.
Mwandishi wa BBC aliyeko Cape Town Afrika Kusini
Pumza Fihlani,anasema mavazi hayo ya wabunge wa EFF yalikuwa ya kipekee
kwani wenzao walikuwa wamevalia mavazi ya kifahari na suti
zinazotengenezewa ughaibuni.
Mbunge wa EFF Floyd Shivambu
" hatimaye wanyonge wamepata waakilishi katika bunge."
Awali wabunge hao waliimba kwa shangwe na
kucheza densi wakizunguka sanamu ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo hayati
Nelson Mandela .
Hata hivyo mwandishi wetu anasema kuwa idadi yao ndogo ambayo ni takriban asilimia 6% ya wabunge 400 haitawaruhusu kupitisha miswaada waliowaahidi wapiga kura wao.
Chama tawala cha ANC kilipata asilimia 62% ya
kura zote huku chama cha Democratic Alliance (DA) kikizoa asilimia 22%
ya kura zote .
Kikao hicho cha bunge kilikuwa mahsusi
kuwaapisha wabunge wapya hata hivyo rais Jacob Zuma anatarajiwa
kuapishwa siku ya jumamosi
No comments:
Post a Comment