Advertisements

Saturday, July 26, 2014

KIKONGWE AUWA KIKATILI KWA KUKATWA NA MAPANGA

Na Mohab Dominick
Shinyanga
July 25,2014


Kikongwe sayi (75)mkazi wa kijiji cha mwagata kata ya mwamalili manispa ya shinyanga  ameuwa  kikatili  kwa kukatwa na mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na kufariki dunia.

Kamanda wa polis mkoa wa shinyanga justu kamugisha amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa tano za usiku  kwa kikongwe huyo .

Akifafanua zaidi kamanda alisema kuwa  wakati kikongwe huyo amelala na wajukuu wake wawili  ghafla  alivamiwa na watu wawila ambao akuwafahamu na kumcharanga na mapanga.
.
Aidha  kamanda alisema kuwa walimcharanga sehemu mbali mbali za mwili wake ikiwemo shingo ,mabenga ,ali ambayo ilipelekea mauti yake kikongwe huyo .joel machia (45)mkazi wa mwamalili  anashikiliwa kwa tuhuma hizo na kwamba uchunguzi wa jambo hili unaendelea .

Kamanda justu  pia amesema kuwa  jeshi la polisi katika uchunguzi wa awali limebaini kuwa chazo cha ugomvi huo ni kugombea mashamba .

Aidha mkoa wa shinyanga umekuwa na matukio ya mara kwa mara ya ukatili wa vikongwe katika mkoa huo jambo ambalo linatia shaka maisha yao kwa  mwezi huu ni kikongwe wa 4 tiali wamekwisha uawa kwa dhima hiyo ya mashamba na uchawi.

No comments: