ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, July 9, 2014

MAMIA WAJITOKEZA KUMZIKA BONDIA SADAT MIYEYUSHO KINONDONI DAR

Baadhi ya mabondia Makocha pamoja na wadau wa mchezo wa ngumi wakiungana pamoja wakati wa msiba wa bondia Sadat Miyeyusho aliezikwa leo katika makaburi ya FM Kinondoni Dar es salaam 
Bondia wa siku nyingi Koba Kimanga akiwa amemeba jeneza lenye mwili wa marehemu Sadat Miyeyusho kwenda kuzika katika makaruri ya FM Kinondoni Dar es salaam
Mabondia Nassibu Ramadhani na Fransic Miyeyusho wakiwa katika msiba wa bondia mwenzao Sadat Miyeyusho 
Kocha wa Ngumi Cristopher Mzazi akiwa kabebwa kwenye poikipiki tayali kwenda kuzika
Mamia ya waombelezaji wakiupereka mwili wa marehemu Sadat Miyeyusho kuzika 
Baadhi ya waombelezaji wakiwa na jeneza lenye mwili wa marehemu Sadat Miyeyusho kwa ajili ya kupereka makaburi ya FM Kinondoni kuzika
Waombelezaji wakiwa wanazika mwili wa marehemu Sadat Miyeyusho katika makaburi ya FM Kinondoni 
Baadhi ya waombelezaji wakiwa makaburini 

Na Mwandishi Wetu
MAMIA ya wakazi wa jiji la Dar es salaam wamejitokeza katika maziko ya bondia Sadat Miyeyusho

yaliyofanyika katika makaburi ya FM Kinondoni Dar es salaam

bondia huyo aliefariki kwa ajali ya pikipiki juzi amezikwa jana katika makaburi hayo ya Kinondoni

Historia fupi ya marehemu inaonesha kuwa alianza ngumi mwaka 2006 ambapo mpambano wake wa kwanza katika ulimwengu wa masumbwi kacheza na Adam Yahya na kushinda kwa point mpambao uliofanyika katika ukumbi wa
DDC Mlimani Park
mpambano wake wa mwisho katika maisha yake ya mchezo wa ngumi ni mwaka 2012 alipopambana na Issa Nampekecha katika ukumbi wa
Friends Corner Hall na kupoteza kwa point
bondia huyo ameshacheza na mabondia wanaotamba kwa sasa kama Ramadhani Shauli na Juma Fundi ambao alisha wai kuoneshana nao umwamba katika uringo


Bondia huyo ameacha mke na watoto
mungu awape subra familia ya marehemu pamoja wa wafiwa wote katika kipindi hiki cha msiba wa mpendwa wetu Sadat Miyeyusho
mbele yake nyuma yetu

No comments: