Advertisements

Saturday, July 26, 2014

NAKANUSHA HABARI ZA KUWA MIMI NI MBAGUZI WA DINI – ASHA NYANG’ANYI

       

Watanzania wote mliosoma habari za uzushi kuwa Mimi ni mbaguzi wa Dini, habari hizi zimekuwa zikisambazwa Katika mitandao tofauti ya simu, Jamii forum na Facebook na baadhi ya wagombea wa uongozi hapa DMV. Simpigii debe mgombea uongozi yeyote kwani mimi ni Katibu wa Tume ya uchaguzi hapa DMV na nina haki ya kukanusha habari hizi zisizo za ukweli na zenye nia ya kunichafulia mahusiano niliyoyajenga na Watanzania wenye Imani ya dini tofauti tangu nilipokuja nchi hii kama mtoto wa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mheshimiwa Balozi Mustafa Nyang’anyi. Kama familia tumekuwa na ushirikiano na Watanzania wa Imani za dini zote kwa kipindi chote mzazi wangu alipokuwa hapa kuanzia mwaka 1995 to 2002 kwani shughuli zote za kijumuiya zilikuwa zikifanyika nyumbani kwa balozi na hapakuwa na ubaguzi wowote wa kidini na wale mliokuwepo miaka hiyo mtakubaliana nami na nikaendelea na ushirikiano huo hadi leo hii. Kwa wale wasionifahamu haya ndiyo malezi niliyopata kutoka kwa wazazi wangu.


MCHANGO WANGU KWA JUMUIYA YETU HAPA MAREKANI

1. Nimekuwa Mwanakamati wa jumuiya ya watanzania tangu Jumuiya hii ifufuke mwaka 2012. Nimefanya kazi na viongozi wa ngazi zote, kuanzia  Bodi, na Executives. (Rais, Makamu wa Rais, Katibu na Mweka Hazina) ambao majority ni wakristo. 


2. Nilikuwa katibu wa Kamati ya maandalizi ya mkutano wa DICOTA hapa Washington DC ambapo sherehe hizi ziliunganika na sherehe za miaka 50 ya UHURU wa Tanzania na tulikuwa waislamu 2 katika Kamati ya WATU 15. Tulishirikiana na uongozi wa juu wa DICOTA na Mheshimiwa Balozi Mwanaidi Maajar na maafisa wengi wa ubalozi kufanikisha maandalizi ya sherehe hizi na mkutano ambapo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa Mgeni rasmi.




3. Katibu wa Kamati ya maandalizi ya matamasha ya vijimambo na katika vikao vyetu mimi Ndiyo niliyependekeza kumwalika Rais nmstaafu Ali Hassan Mwinyi kwa Wajumbe na wakaafiki pendekezo hilo. Kamati hii inaongozwa na Baraka Daudi na mimi ni mwanamke pekee na tupo waislamu watatu. Na nimefanya kazi kwa Karibu na maafisa wa ubalozi, Wahadhiri wa lugha ya Kiswahili na wajasiriamali wa hapa Marekani wa Imani tofauti katika kufanikisha Tamasha la vijimambo mwaka jana na tupo tunatayarisha tamasha lingine mwaka huu na wengi mmeishaona matangazo. 






4. Mratibu Ms. Tanzania USA pageant. Nimefanya kazi kwa Karibu na founder mama Winny Casey kuandaa haya maonyesho kwa mara ya kwanza hapa Marekani. Ni muislamu pekee katika Kamati yote na nimeshirikiana na mabinti zetu walioshiriki kwa Mara ya kwanza, Wanakamati wasio watanzania na wasio waislamu. Tuliwapokea toka states mbalimbali na Mimi niliwahost wasichana  wote waliotoka out of state na wa hapa kuwatoa usiku kwenda kuona mji wetu na pia waliotoka nje ya mji on thanksgiving dinner mwaka Jana. Wale waliofika Kwangu watatoa ushahidi.





5. NIMEJITOLEA kufundisha darasa la Kiswahili kwa watoto wa kitanzania hapa DMV. Darasa hili hukutana kanisani. Watoto wengi wa Shule hii si waislamu na walimu wote si waislamu (I'm the only MUSLIM teacher) na tumefanya kazi pamoja bila matatizo yeyote. 
http://lukemusicfactory.blogspot.com/2013/04/darasa-la-kiswahili-leo-jumamosi-dmv.html?m=1


6. Nimeshiriki misa katika Makanisa tofauti, nimepika na kusimama kuserve vyakula kwenye Matukio mbalimbali ya marafiki zangu Kama ubarikio wa watoto wetu. Vipaimara na Misiba yaliyofanyika kanisani. 



7. TAMCO ni umoja wa waumini wa Dini ya kiislamu na Mimi ni mwanachama wa TAMCO na nipo kwenye Kamati ya uongozi. Nimeshirikiana na waislamu wenzangu katika mambo ya Ibada kwani nimezaliwa na kulelewa katika Imani ya Dini ya kiislamu na ninaipenda Dini yangu. Nimeshiriki katika maandalizi ya sikukuu zote za kidini, Nimeshiriki katika maandalizi ya mfungo wa Ramadhan na katika mambo yote yanayohusu Dini yetu na nimewakaribisha marafiki zangu wasio waislam Kuja kushirikiana nasi katika sherehe zote za kiislamu. TAMCO imekaribisha watanzania wote bila kujali imani zao.
http://www.jestina-george.com/2014/07/libe-aungana-na-iftar-ya-tanzania.html


8. Nimehudumia jamii ya Wanawake wa Kitanzania bila kujali Imani zao, sasa hivi ninaandikisha kila mwanamke wa Kitanzania anayeishi hapa DMV kupata huduma ya bure ya mammogram na kampuni moja hapa DC ambaye founder wake ninafahamiana naye na si muislamu, na tumeisha anza kuweke mipango ya kwenda Tanzania next summer for medical mission trip kutoa huduma ya matibabu na semina ya mambo tofauti yanayohusiana na afya. Nimeshiriki katika makongamano ya wanawake na kila kitu kinachomhusu mwanamke wa dini yoyote hapa DMV.

HITIMISHO:

Hayo yote yanayosemwa kuwa mimi ni mbaguzi wa dini si ya kweli na vidhibiti hivyo hapo juu. Nimetumikia na kujitolea elimu yangu, uzoefu na malezi niliyopata maishani katika kujenga jumuiya yetu. Ushauri wangu kwa wagombea wa uongozi ni kuacha kuandika habari zisizo na uhakika kuhusu wanajumuiya na kuwaharibia mahusiano na mtazamo wao kwa jamii bali mjikite katika kutangaza mchango wako ulioutoa kwa wanajumuiya au utakaoutoa kwa wanajumuiya. Hizi campaign ni za kuwa kiongozi wa kuhudumia jamii bila kipato chochote. Tuonyeshe heshima na upendo baina yetu na si kuandika mambo yanayohatarisha upendo na kuleta mpasuko kwenye jumuiya yetu.

Shukran,
Asha Nyang’anyi.

Kama una comment nitumie ashany2@yahoo.com