Advertisements

Thursday, August 21, 2014

Bomu larushwa ndani ya basi Kigoma, watatu wauawa, sita wajeruhiwa



Picha ni Basi la Luhanga lilivyoungua moto huko Kibondo, Kigoma JUNE 2013 PICHA NA MAKTABA picha hii sio basi lililotupiwa bomu.

Kigoma. Watu watatu wamekufa akiwepo mtoto mchanga na wengine sita kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria (Hiace) kurushiwa bomu na watu wasiojulikana huko Kasesema, Kigoma alfajiri ya leo.

AKithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Wilaya ya Buhigwe (OCD), Samwel Utonga alisema basi hilo lilikuwa likotokea Kilelema kwenda Kasulu Mjini ambapo watu hao walilirushia kitu kinachoaminika kuwa ni bomu.

Taarifa kutoka Hospitali ya Muyama zinazema majeruhi hao wamehamishwa toka hospitalini hapo na kupelekwa Hospitali ya Kasulu baada ya hali zao kuwa mbaya.

 Mwananchi

No comments: