1944 URSULA SABINUS KWEKA 2014
Kwa niaba ya Familia ya Mzee Sabinus Kweka, napenda kutoa
shukrani za dhati kwa matendo, majitoleo na upendo wenu usiku na mchana kwa
ajili ya mama yetu Mpendwa URSULA KWEKA kuanzia ugonjwa hadi kifo chake ambacho
kilitokea usiku wa kuamkia tarehe 30/07/2014 na kuzikwa tarehe 05/08/2015
kijijini kwake NARUMU,wilaya ya HAI,mkoa wa KILIMANJARO. Kwa kuwa siyo rahisi
kumshukuru kila mmoja kipekee, tunaomba mpokee nyote shukrani hizi kwa moyo
mkunjufu. Kweli tumeuona utukufu wa Mungu. Ila tutakuwa Wachoyo wa fadhila kama
hatutashukuru watu au vikundi vifuatavyo:-
1.
Uongozi wote wa Mkoa wa Kilimanjaro ukiongozwa
na Mkuu wa Mkoa,Mhe.L.GAMA kwa kuwa nasi
siku ya Mazishi
2.
Madaktari na Wauguzi wote wa Hospital za
Dr.Mohamed,Selian – Arusha,pamoja na Bugando Medical Centre alikofia marehemu
kwa huduma zao za kuokoa maisha ya marehemu bila mafanikio.
3.
Majirani wa zamani wa Capripoint na wakazi wote
wa Calfonia Nyegezi alikokuwa akiishi Marehemu
4.
Ndugu,Jamaa na Marafiki popote walipo hasa
wanarumu wa Mwanza na Watanzania waishio Marekani kwa michango yao ya hali na
mali pamoja na maombi
5.
Vikundi mbalimbali vilivyosaidia kuomboleza
msiba K.m Jumaki, Umamwa,Ukiki,Tupendane,wafanyakazi wa Benki kuu Mwanza,Kweka
Law Chambers,Kituo cha Utafiti Selian,Kwaya ya Mt.Augustino ya Parokia ya
Mkolani kwa mkesha siku zote za maombolezo.
6.
Mwisho,wanavijiji wote wa NARUMU,
Waombolezaji wote toka sehemu mbalimbali
za Nchi, Mapadri na Masista wote walioshiriki Ibada ya
Mazishi…………………………………………………………….
RAHA YA MILELE UMPE Eee BWANA………………………………
“HERI KUIENDEA NYUMBA YA MATANGA, KULIKO
KUIENDEA NYUMBA YA KARAMU KWA MAANA HUO NDIO MWISHO WA WANADAMU WOTE” MHUBIRI
7:2
No comments:
Post a Comment