Advertisements

Friday, September 19, 2014

FRELIMO WATUA NCHI TANZANIA NA KUKUTANA NA UONGOZI WA CCM TAIFA,MWIGULU NCHEMBA AZUNGUMZA NAO

Kushoto ni Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania,Katikati Mh:Mwigulu Nchemba Naibu katibu Mkuu CCM Bara na Kulia ni Bi,Nyeleti Mondlane ambaye ni Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha FRELIMO Nchini Msumbiji.Ujumbe huu kutoka Msumbiji ulitembea Ofisi za CCM lumbumba jana Tar.18/09/2014 CCM na FRELIMO ni Vyama rafiki na vyote vimeshiriki katika harakati za Ukombozi.Hivi sasa Nchini Msumbiji wapo kwenye Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa RAIS,ambapo FRELIMO imemsimamisha Filipe Nyussi kuwa Mgombe URAIS.Kihistoria Nyussi amepata kusoma Kusini mwa Tanzania mji wa Tunduru na amepata mafunzo ya kijeshi Kambi ya Nachingwea.Naibu Katibu Mkuu CCM Bara akimvalisha skafu ya Tanzania Bi. Nyeleti Mondlane kutoka MSumbiji chama cha FRELIMONaibu Katibu Mkuu CCM Bara Mh,Mwigulu nchemba akiwa katika picha ya Pamoja na Ujumbe kutoka Msumbiji-FRELIMO uliofika Ofisi ndogo za Chama cha Mapinduzi Lumumba Dsm kwaajili ya kuzingumza mambo mbalimbali ikiwamo Uchaguzi wa Msumbiji unaotegemewa kufanyika mwaka huu.

3 comments:

Mbele said...

Kuna jambo ambalo sherti wa-Tanzania walipambanue vizuri, muda wote. Wakati wa harakati za ukombozi Msumbiji, hapakuwa na CCM, bali TANU. Uhuru wa Mozambiki ulipatikana mwaka 1975, wakati CCM ilianzishwa mwaka 1977.

Imejengeka tabia Tanzania ya kuipa CCM maisha marefu kuliko ukweli ulivyo. Kwa mfano, ni kawaida kabisa kwa wa-Tanzania kusema kwamba CCM imekuwa madarakani miaka Zaidi ya hamsini. Inasahaulika kuwa chama kilicholeta uhuru si CCM bali TANU.

Hilo ni angalizo tu, ili tunaposoma habari kama hii ya FRELIMO na CCM tusijichanganye. Tukumbuke historia ya TANU, na tuzingatie kuwa hizo habari za CCM zinaanzia mwaka 1977.

Anonymous said...

MDAU NAKUUNGA MKONO SANA KATIKA HILI SABABU MIMI 1974 NILIIMBA SANA NYIMBO ZA UKOMBOZI KUHUSU ZIMBZBWE,MOZAMBIQUE,SOUTH AFRICA NA NAMIBIA.WAKATI HUO NILIKUWA TYL yaani TANU Youth Leage. TANU ndilo chama la ukombozi. Labda hawa watu waZANU PF hao walipiganiwa pia na CCM. Watanzania tujue jinsi ya kupambanua civics na historia kimaandishi

Anonymous said...

Tanu CCM ndiyo wale wale tu. Ni jina tu limebadirika. Watu na itikadi ni zilezile. To me if I blame ccm then I blame Tanu too. If I praise Tanu I praise ccm on the other hand. Viongozi wote wakuu wa Tanu si ndiyo walio ingia ccm? Sasa angalizo lipi tena unaweka? Tofauti ni majina tu dada hakuna kingine.