Advertisements

Wednesday, April 1, 2015

Wanasheria naombeni msaada

Nafikiri wote tumesikia na kusoma kwenye mitandao mbali mbali kuhusu ndoa ya Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr. Reginald  Mengi na former Bongo Flava Artist Jacqueline Ntuyabaliwe (K-Lynn). Ndoa hiyo amabayo inasemekana kufungwa katika visiwa vya Mauritius na watu wachache sana wameweza kuhudhuria tukio hilo; katika hao watu wachache inasemekana hakuna mtoto wake hata mmoja (kutoka kwa ndoa yake na mke mkubwa) ambaye alikuwa hapo kushuhudia tukio hilo. Pia vile vile hakuna ndugu wala jamaa wa karibu kabisa wa Dr. Mengi ambaye alialikwa  kushuhudia ndoa hiyo! Hili swala limenikumbusha kitu ambacho kilishawahi tokea miaka ya huko nyuma ambacho kilipelekea Mr. Mengi kuita waandishi wa habari na kukanusha tuhuma hizo.

Mwaka 2009 kuna picha zilitumwa mitandanaoni ambazo zilionyesha Dr. Mengi na mdada aitwaye Lilian Kimaro ( wengi tuliziona) pamoja na watu wengine wakiwa kwenye sherehe fulani.  Mavazi yao na mazingira ya party yalikuwa yakiashiria watu hao wawili na wengine walio kuwepo kwenye picha kuwa ilikuwa ni sherehe fulani muhimu. Wajuzi wa habari wakitoa taharifa kwamba by then Mr. Mengi now ni "Dr. Mengi" amefunga ndoa na mrembo huyo (Lilian Kimaro), kitu ambacho Dr. Mengi alikuja akakanusha kwa kusema ni kuwa ni uzushi tuu wakutaka kumchafulia jina, pia akahusisha jambo hilo na jitihada zake za kupinga ufisadi. Unaweza kujikumbusha story hiyo kwa link hizi zifuatazo:-

Kusoma zaidi bonyeza HAPA

11 comments:

Anonymous said...

This is a private/family matter. What's your question????

Anonymous said...

Sasa swali lako kwa wanasheria ni lipi? Hii imekaa udakuudaku.

Anonymous said...

Hizi hela hizi!!!,binti na babu yake.

Anonymous said...

Mmmmh! nyie mgesoma mpaka mwisho mngeona maswali mbona wengine tumeona?

Anonymous said...

Nimesoma maswali yaliyoulizwa na majibu yake ni yafuatay.
1. Dr Mengi na K-Lynn wanahaki ya kufanya watakavyo ni maisha yao
2. Unajuaje kama Mengi hakuachana na mke wake wa kwanza?
3. Usichanganye dini na sheria. Kwa sheria ndoa yoyote inavunjika, kama mmoja wa wanandoa ataamua hivyo. Maswala ya dini Ugeuliza kanisani hulko walikofungia
4. Ndoa kufungwa bila kuwa na watu wengi ni uamuzi binafsi si lazima watu wengi waalikwe au ulitaka kupata trip ya bure? Watoto wa mengi aliozaa na mkewe mkubwa wanajua sababu zao kwanini hawakuhudhuria, wewe haya yanakuhusu nini?
5.Urithi unategemea na hati ya mirathi. Mengi anaweza kumrithisha yeyote amtakaye, sio lazima awe mke, mtoto, au mjomba.
5. Is this really any of your business?

Anonymous said...

Hilo ndio tatizo la waTZ, haya ni maisha ya mtu binafsi wewe yanakuhusu nini mpaka uombe eti tena wanasheria wakusaidie.. what for? Unapata nini out of this?

Unafikiri Jaqueline hayajui yote hayo kabla hajafanya maamuzi ya kuolewa na Dr. Mengi?!

Hebu wacheni wivu... Muacheni ale maisha mtoto wa watu!!!!!!!

Anonymous said...

Sijaona swali nimesoma mpaka mwishi naona maelekezo/utoaji ya taarifa tu.

Anonymous said...

Kweli tutafute hela, mtoto mkali kakubali kuolewa na babu daa!!

Anonymous said...

Lazima huyu atakuwa ni MKE aliyeachwa au ndugu zake wa karibu! Labda nikujibu tuu hilo la mirathi, Mengi akifa Kylnn ndio IPP. Sasa kajinyonge kabisa.. tehe tehe th heehee!

Anonymous said...

Tuwatakie maisha na malezi mema.kama ni dini Mbona mfalme daudi alimpata Abishagi akiwa miaka mia. na zaidi .Dr Mengi amefanya mengi mazuri na Mungu amembariki kumpa watoto na klynn
n

Anonymous said...

Klynn amechaguliwa na kubarikiwa kuingia katika familia ya Dr Mengi kama Esta alivyokubalika na Mungu ili awasaidie Wayahudi.She will be an ambassador of peace,harmony and happiness and a pillar to lean on for Dr Reginald Mengi at old âge.