Mhe. Waziri Fatma Fereji kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akizungumza kwa niaba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kikao Maalum cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Jumatatu ambapo wakuu wa nchi na wawakilishi wa serikali kutoka nchi 193 walikutana kutathimini Mpango wa Utekelezaji walioupitisha miaka 20 iliyopita huko Cairo, Misri kuhusu uboreshaji wa maisha ya watu na masuala yahusuyo Idadi ya Watu. Mhe. Fereji ni sehemu ya Ujumbe wa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika Mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Mhe. Waziri Fatma Fereji akiwa na Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi na Naibu wake, Balozi Ramadhan Mwinyi wakati wa ufunguzi wa Kikao Maalum wa ICPD ambapo Waziri Fereji aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo.
Kutoka kushoto ni Balozi Ramadhan Mwinyi, Waziri Fatma Fereji wakiwa na Mwakilishi kutoka Ofisi za UNFPA ambaye aliwahi pia kufanya kazi nchini Tanzania akimpongeza Waziri baada ya kutoa mchango wa Tanzania na kulia kabisa ni Dkt. Joyceline Kaganda
Na
Mwandishi Maalum, New York
Kikao
Maalum kilichowakutanisha Viongozi wakuu wa Nchi
na wawaskilishi wa serikali kwa
lengo la kutathmini hatua ambazo
zimechukiliwa na serikali katika kuboresha maisha ya watu na masuala ya
idadi ya watu kwa kipindi cha miaka 20
iliyopita kimefanyika siku ya Jumatatu hapa Umoja wa Mataifa.
Ujumbe
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano huo, umeongozwa na Mhe. Fatma Fereji Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa
kwanza, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Mhe. Fereji ni sehemu ya Ujumbe wa Mhe.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika Mkutano wa 69 wa Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa.
Mwaka 1994 nchi wanachama wa 179 wa Umoja wa
Mataifa walikutana katika Mkutano wa
Kimataifa wa Idadi ya Watu na Maendeleo ( ICPD)uliofanyika mjini Cairo ambapo
walithibisha ahadi zao ambazo pamoja na mambo mengine zilikuwa za kuhakikisha
kuwa haki na ustawi wa watu unakuwa msingi mkuu katika suala zima la maendeleo.
Mkutano
huo ( 1994)ulitoa Mpango wa Utekelezaji
uliosisitiza umuhimu wa kulinda haki za binadamu, hasa haki za wanawake na
vijana, kuwekeza katika afya na elimu, kuendeleza usawa wa kijinsia na
kuwawezesha wanawake, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya na
haki za uzazi.
Miaka
20 baadaye nchi wanachama ambazo sasa ni 193 wamekutana katika Mkutano huo wa jumatatu na ambao
ulikwenda hadi usiku kutathimini
mpango huo wa utekelezaji, kupima
matokeo yake , changamoto zake na kurejea ahadi walizotoa mwaka 1994.
Karibu kila mjumbe aliyepanda jukwaani kuzungumza alielezea kile ambacho serikali yake imetekeleza katika
kuboresha afya ya wanawake, watoto, upatikanaji wa huduma zote za msingi zinazohusu afya, elimu, uboreshwaji wa haki za
msingi za makundi mbalimbali ya jamii, fursa
sawa za kijinsia na kupunguza idadi ya watu maskini.
Pamoja
na kuelezea mafanikio wajumbe hao pia
walielezea changamoto mbalimbali zikiwamo za uhaba wa raslimali fedha,
wataalamu wa kutosha, kuendelea kuwapo
kwa watu maskini, vifo vitokanavyo na
uzazi , vifo vya watoto wachanga, ndoa na mimba za utotoni na magonjwa kama
vile malaria, kifua kikuu, ukimwi na
sasa Ebola.
Akizungumza
kwa niba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Waziri Fatma Fereji, pamoja
na kuelezea maeneo ambayo Tanzania imefanikiwa
kuyatekeleza vema katika kipindi hicho cha miaka 20 amesema,
umaskini bado ni tatizo kubwa na ambalo limeendelea kuchangia pamoja na mambo mengine ndoa za utotoni.
Akayataja
baadhi ya maeneo ambayo Tanzania
imefanya vizuri kuwa katika Malengo ya
Maendeleo ya Millenia namba mbili, tatu na nne ambayo yamepata mafanikio ya kuridhisha hata kabla
ya mwaka 2015.
Akaeleza
kuwa, Tanzania bado inakabiliwa na vifo vya watoto vinavyotokana na magonjwa
yanayoweza kuzuilika kama vile,
malaria, kuharisha na kifua
kikuu. Hata hivyo amesisitiza kuwa
serikali inaendelea na juhudi mbalimbali zinazolenga kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu
changamoto zilizobakia.
Akaitaka
Jumuiya ya Kimataifa kuhakikisha kwamba
vipaumbele vya kitaifa katika eneo zima la ustawi wa watu na maendeleo vinapewa
umuhimu na hususani katika kipindi hiki ambacho jumuiya hiyo ya kimataifa
imejikita katika maandalizi ya malengo
mapya ya maendeleo endelevu baada ya 2015.
Akasisitiza
kuwa ni vema pia Jumuiya ya Kimataifa ikaendelea kuyafanyia kazi maeneo ambayo
bado ama
yatakuwa hayajakamilika ifikiapo mwaka 2015 lakini vile vile yasiachwe njiani bali yawe sehemu ya
maeneo yatakayoshughulikwa baada
ya 2015.
Pamoja
na wakuu wa nchi na wawakilishi wa
serikali kuzungumza katika mkutano huo,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, Rais wa Baraza Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa,Bw. Sam Kutesa na
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko
wa Idadi ya Watu wa Umoja wa Mataifa ( UNFPA) Babatunde Osotimehin nao
walizungumza mwanzoni mwa mkutano huo.
No comments:
Post a Comment