Familia
ya Captain Narcis Mapunda wa Mikocheni B (TPDC) Dar es salaam, kwa masikitiko
na huzuni wanatoa taaifa ya msiba wa mtoto wao mpendwa;
ELIAS NARCIS MAPUNDA
Kifo hichi ilichotokea siku ya Ijumaa tarehe 28
November 2014 hapa jijini Dar es salaam. Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani
kwa Baba mzazi Captain Narcis Mapunda, pale mikocheni, Nyumbu Street (pandisha mtaa wa mikocheni Wariob tokea Mwai
Kibaki Rd, baada ya Kanisa la Mt Martha ingia mtaa unaofuata kulia).
Maandalizi ya awali yanalekea kuwa na ratiba
ifuatayo ya mazishi; mazishi yatafanyika kinondoni Makaburi ya Jumuiya ya
Madola (ndani ya ukuta) siku ya alhamisi tarehe 4 December 2014 majira ya saa
10 jioni (1600 hrs). Awali ya hapo kutakuwepo
misa fupi, chakula pamoja na za heshima za mwisho nyumbani kwa Capt
Mapunda, ikifuatiwa na misa maalum pale jirani kanisa la Mt Martha. Ratiba ya shughuli zote inatarajiwa kuanza
saa 4.30 asubuhi ya siku hiyo (1000hrs).
Habari za msiba huu ziwafikie wana-Mapunda popote
pale walipo pamoja na nduguwote na marafiki.
No comments:
Post a Comment