Advertisements

Sunday, February 1, 2015

DIAMOND AMJIBU KWA VITENDO EX WA ZARI

Diamond akiwa kwenye baiskeli huku Zari akiwa kwenye BMW X6.

Baadhi ya post za King Lawrence Instagram akimkejeli Diamond.

STAA wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’, ameamua kumjibu kwa vitendo anayedai kuwa aliwahi kuwa mpenzi wa mwandani wake wa sasa, Zarinah Hassani ‘Zari’, King Lawrence ambaye amekuwa akimtupia maneno ya kumtusi na kejeli mitandaoni.
Diamond akipozi na mpenzi wake Zari.

King Lawrence ambaye ni binamu wa aliyekuwa mume wa Zari aliyezaa naye watoto watatu Ivan amekuwa akimnanga Diamond mitandaoni hasa Instagram kama mtu aliyefulia na hana fedha ambapo siku za nyuma aliwahi kuandika post akisema kuwa yuko tayari kumpatia kiasi cha Usd 40,000 sawa na zaidi ya shilingi milioni 71 Diamond aachane na Zari.

Katika kuonyesha kuchoshwa na tabia hizo za King Lawrence, Diamond ameamua kutupia picha yake akiwa amepanda baiskeli huku mpenzi wake Zari akiwa katika mkoko mkali aina ya BMW X6 akimaanisha kumkebehi mtu huyo kuonyesha kuwa hana kitu ila anaomba penzi kwa mtoto mkali aliye kwenye BMW.

GPL

2 comments:

Anonymous said...

Huyo anaye jiita mfalme Lawrence mshamba tu. Mwenye pesa hajigambi

Anonymous said...

Hawajui Diamond ni mtoto wa Tandale???He had lived and seen it all!!!!The low of the lowest and the high of the highest!!!!LOVE U BROTHER DIAMOND PLTNMZZZZZZ!!!!