ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, February 26, 2015

Rais Kikwete amtembelea Rais Kaunda Lusaka

Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt.Kenneth Kaunda akimkaribisha nyumbani kwake Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete huko kijijini kwake Mkango Barracks, State Lodge nje ya jiji la Lusaka leo Dkt. Kaunda ambaye alimwalika Rais Kikwete alifanya naye mazungumzo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka shada la maua katika kaburi la mke wa Rais wa Kwanza wa Zambia Mama Betty Mutinkhe Kaunda huko Mkango Barracks,State lodge, nje ya jiji la Lusaka leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha wageni nyumbani kwa Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt.Kenneth Kaunda(aliyesimama akiangalia) leo wakati alipomtembelea mwasisi wa taifa hilo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais wa kwanza wa Zambia Dkt.Kenneth David Kaunda nyumbani kwake Mkango Barracks,State lodge, nje ya jiji la Lusaka leo
Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt.Kenneth Kaunda akimpa zawadi Rais Dkt.Jakaya Kikwete.
Rais wa Kwanza wa Zambia Mzee Kenneth Kaunda akimsindikiza Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiagana wakati akijitayarisha kuondoka
Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiagana na Rais wa Kwanza wa Zambia Mzee Kenneth Kaunda mara baada ya kumtembelea na kufanya naye mazungumzo leo(picha na Freddy Maro)

No comments: