Wednesday, March 11, 2015

43 WAAPISHWA KUWA MANAIBU WASAJILI WA MAHAKAMA YA TANZANIA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila akimwapisha Mhe. Lenatus Ishengoma (kulia) kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam. Wanaoshuhudia kiapo hicho ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Othman Chande (kushoto) na Mhe. John Kahyoza, Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila akimkabidhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwongozo wa utendaji kazi wa Mahakama Mhe. Zahara Abdallah Mlacha mara baada ya kumwapisha kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
Mhe. Elizabeth Mkwizu akisaini hati ya kiapo cha kuwa Naibu Msajili wa Mahakama mbele ya Jaji Kiongozi Mhe. Shaaban Ali Lila baada ya kuapishwa leo leo jijini Dar es salaam.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila akimwapisha Mhe. Hussein Shaban Mushi kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika viwanja vya Mahakama ya Rufani leo jijini Dar es salaam.
Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Hussein Shaaban Mushi akipokea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwongozo wa utendaji kazi wa Mahakama kutoka kwa Jaji Kiongozi Mhe. Shaaban Ali Lila mara baada ya kuapishwa kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
Mhe. Isaya Khalfan (kulia) akila kiapo cha kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila (kulia) leo jijini Dar es salaam.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila (aliyekaa) akisaini kiapo cha Mhe. Angela Maria Thei (kulia) aliyeapishwa kuwa Msajili wa Mahakama ya Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika viwanja vya Mahakama ya Rufani leo jijini Dar es salaam. Anayetazama kiapo hicho ni Msajili wa Mahakama kuu ya Tanzania Mh. John Kahyoza (katikati).
Manaibu Wasajili wa Mahakama ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji Wakuu wa Mahakama Tanzania wakiongozwa na Jaji Mkuu Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati waliokaa mbele) na Jaji Kiongozi Mhe. Shaaban Lila (kulia waliokaa mbele).

(Picha na Aron Msigwa –MAELEZO)

No comments: