Advertisements

Wednesday, March 4, 2015

Hatimaye Profesa J atangaza rasmi kugombea ubunge jimbo la Mikumi

Profesa J ametangaza rasmi kuwa atagombea nafasi ya ubunge kwenye jimbo la Mikumi mkoani Morogoro.
Akiongea na 255 ya Clouds, rapper huyo ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule, amesema:
Unajua nimeamua kugombea jimbo la Mikumi kwa kuwa hapa ni nyumbani. Wazazi wangu waliishi hapa kwa muda mrefu maana babu yangu alihamia hapa kama miaka 58 iliyopita. Baba pia yupo hapa japo wao ni watu wenye asili ya mkoa wa Ruvuma. Kwahiyo nimeona nimekuwa nikiimba siasa sana naona huu ni muda wa kufanya vitendo zaidi."

No comments: