Advertisements

Saturday, March 28, 2015

MECHI YA URUSI NA MONTENEGRO YATIBUKA

Wachezaji wa Montenegro

Mechi ya kufuzu ya kuwania kombe la taifa bingwa barani Ulaya kati ya urusi na Montenegro ilisitishwa baada ya wachezaji kutoka timu zote kupigana uwanjani.

Awali mechi hiyo ilikuwa imesitishwa kwa dakika 30 baada ya mlinda lango wa Urusi kugongwa na kifaa na kisha kupelekwa hospitalini.

Wakati Urusi ilipopoteza penalti katika cha kipindi cha pili wachezaji na maafisa kutoka pande zote walianza kupigana.

Kisha mchezaji mwingine wa Urusi aligongwa wakati vifaa zaidi viliporushwa uwanjani hatua iliyomfanya refa kusimamisha mechi hiyo.

Hakuna timu iliyokuwa imefunga bao wakati huo na haijulikani hatua ambayo itachukuliwa na shirikisho la soka barani ulaya.

No comments: