Mwathiriwa ambaye alikuwa mja mzito wa miezi saba anatarajiwa kupona kufuatia upasuaji lakini mtoto alikufa baada ya kuvhomwa kisu.
Mwanamke huyo mjamzito alikuwa akimtembelea mshukiwa ili amnunulie mwanawe nguo ambazo zilikuwa zimetangazwa katika katika soko la mtandao la Craigslist.
Mshukiwa Dynel Catrece Lane alimpoteza mwanawe wa miezi 19 muongo mmoja uliopita alipokufa maji katika kidimbwi cha samaki
Mwathiriwa mwenye umri wa miaka 26 alikua akitaka kununua nguo hizo wakati aliposhambuliwa siku ya jumatano.
Wakati alipoingia katika nyumba hiyo alishambuliwa na kupigwa kabla ya mwanawe kutolewa kutoka tumboni'',Afisa mmoja wa Polisi Jeff Satur alisema.
Mwathiriwa alifanikiwa kupiga simu ya dharura lakini alipatikana katika hali mbaya wakati maafisa walipowasili. BBC
1 comment:
BBC please do spell check, Quality is better than quantity. Thanks
Post a Comment