Advertisements

Wednesday, March 4, 2015

Naibu Waziri akutana na mgombea uenyekiti wa IPCC na Balozi wa Comoro nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti kwenye Kundi la Wataalam chini ya Umoja wa Mataifa linaloshirikisha wadau kutoka sekta ya umma na binafsi kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi-Intergovernmental Panel on Climate Change-IPCC, Prof. Jean-Pascal Van Ypersele kutoka Ubelgiji ambaye alifika Wizarani kwa ajili ya kumsalimia Mhe. Maalim. Katika mazungumzo yao Prof. Ypersele alielezea dhamira yake ya kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuongeza wataalam kwenye kundi hilo pindi atakapochaguliwa kwenye nafasi hiyo. 
Prof. Ypersele nae akichangia jambo wakati wa mazungumzo yao. Kushoto ni Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe. Koenraad. 
Mazungumzo yakiendelea 
Balozi Adam akisaini Kitabu cha Wageni Ofisini kwa Mhe. Mahadhi 
Prof. Ypersele nae akisaini Kitabu cha Wageni 
Mhe. Mahadhi katika picha ya pamoja na Prof. Ypersele 
Mhe. Maalim akiwa na Prof. Ypersele pamoja Balozi....na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) 
.....Mkutano kati ya Mhe. Mahadhi na Balozi wa Comoro hapa nchini 
Mhe. Dkt. Mahadhi akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Comoro hapa nchini, Mhe. Dkt. Ahamada Al Badaoui Mohamed alipofika kwa ajili ya mazungumzo ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili. 
Balozi Mohamed akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Mhe. Dkt. Mahadhi 
Mhe. Dkt. Mahadhi akifafanua jambo kwa Mhe. Dkt. Mohamed. Wengine ni Bw. Adam Issara, Katibu wa Naibu Waziri na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mambo ya Nje 
Mhe. Dkt. Mahadhi akiagana na Dkt. Mohamed Picha na Reuben Mchome

No comments: