Advertisements

Sunday, March 1, 2015

NAIBU WAZIRI DK.PINDI CHANA AZINDUA MRADI WA 'MPE RIZIKI SI MATUSI' KUMLINDA MWANAMKE DHIDI YA UKATILI KATIKA MASOKO‏

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana (kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa 'Mpe Riziki si Matusi" kumlinda mwanamke dhidi ya ukatili katika masoko wakati akiuzindua Dar es Salaam jana. Mradi huo unaendeshwa na Shirika la Equality for Growth (EfG). Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Ilala, Mkurugenzi Mtendaji wa EfG, Jane Magigita na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Wilaya ya Ilala, Nora Mzeru.
Naibu Waziri Dk.Pindi Chana akihutubia wakati wa uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa EfG, Jane Magigita (katikati), akitoa hutuba fupi mbele ya mgeni rasmi, Naibu Waziri Chana Pinda (kulia). Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Wilaya ya Ilala, Nora Mzeru.
Mkurugenzi Mtendaji wa EfG, Jane Magigita (kushoto), akimkaribisha Naibu Waziri Dk.Pindi Chana baada ya kuwasili kwenye uzinduzi wa mradi huo.
Mmoja wa wadau waliofadhili mradi huo akisalimia wageni waalikwa.
Wanawake wafanyabiashara kwenye masoko mbalimbali wakimsikiliza mgeni rasmi Dk.Pinda Chana. 
Mgeni rasmi Dk.Pindi Chana (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanawake wafanyabiashara masokoni na wadau wengine baada ya kuzindua mradi huo.
Baadhi ya maofisa wa EfG (wenye sare) na wadau wengine wakisakata rhumba kwenye hafla hiyo
Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo (kulia), akicheza ngoma ya kabila ya Wahehe iliyokuwa ikipigwa na kikundi cha Sanaa cha Machozi kilichokuwa kikitoa burudani wakati wa uzinduzi huo.
Hapa ni burudani kwa kwenda mbele.
CREDIT:GPL

No comments: