THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE
HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
RAIS
KIKWETE AUNGANA NA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KUMZIKA KEPTENI JOHN DAMIANO KOMBA
KIJIJINI LITUHI LEO
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumanne, Machi 3, 2015, ameungana na mamia ya waombolezaji kumzika Mbunge wa
Jimbo la Nyasa na msanii mahiri wa muziki nchini, Mheshimiwa Kepteni John
Damiano Komba, kwenye makaburi ya Kanisa Katoliki katika Kijiji cha Lituhi,
Wilaya ya Nyasa, Mkoa wa Ruvuma.
Mara
baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Songea, akitokea Dar es Salaam,
kiasi cha saa tano na robo asubuhi, Rais Kikwete amekwenda moja kwa moja
Lituhi, karibu kiasi cha kilomita 140 kutoka mjini Songea, kwa ajili ya mazishi
ya Mheshimiwa Komba ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC)
ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Rais
Kikwete amejiunga na waombolezaji akiwemo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda kiasi cha saa tisa mchana kwa
ajili ya mazishi ya mmoja wa wasanii ambao walijijengea heshima kubwa kwa
nyimbo zake za uhamasishaji.
Wakati
wa shughuli za mazishi ambazo kidini zimeongozwa na Askofu John Ndimbo wa Jimbo
Katoliki Mbinga, waombolezaji walisomewa salamu za rambirambi ambazo zimetumwa
na Rais wa Pili wa Malawi, Mheshimiwa Bakili Muluzi ambaye sasa amestaafu.
Katika
salamu hizo, Mheshimiwa Muluzi amesema: “Nilimjua Komba kama rafiki na taarifa za
kifo chake cha ghafla zimenistua sana.”
Mwili
wa Marehemu Komba uliteremshwa kaburini saa 9:30 mchana huku ukishuhudiwa na
mjane wa marehemu Salome Komba na watoto wake 11.
Rais
Kikwete ameondoka Lituhi mara baada ya mazishi kurejea mjini Songea kumalizia
ziara yake ya siku mbili ya kikazi mkoani Ruvuma.
Ends
Imetolewa
na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
3 Machi, 2015
No comments:
Post a Comment