Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akifanya ziara ya
kutembelea wagonjwa waliojeruhiwa katika vurugu za kisiasa zilizotokea
siku ya mkutano wa CUF uliofanyika Makunduchi tarehe 29/03/2015.
Baada ya kuwaangalia wagonjwa hao katika mitaa mbali mbali ya Mjini Magharibi ikiwemo mitaa ya Jang'ombe, Muembe Makumbi na Mfenesini, Maalim Seif amesema Chama hicho hakitotoka kwenye mstari na kamwe hakitojitumbukiza kwenye vurugu hizo zilizopangwa kwa malengo ya kukivurugia malengo yake. (picha na Salmin Said, OMKR),
No comments:
Post a Comment