Advertisements

Monday, May 18, 2015

HITIMA YA BABA MZAZI WA MAMA TUNU PINDA YAFANYIKA

TU1
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akifarijiwa na Mke wa makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Seif Iddi katika Sala ya Arobaini ya kifo cha Baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Marehemu Abdallah Rehani iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Mei 17, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
TU2
Sheikh wa mkoa wa Dar es salaam, Alhaji Mussa Salum akizungumza katika sala ya hitima ya marehemu Abdallah Rehani, baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Mei 17, 2015.Kulia ni Waziri Mkuu Mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa katavi, Dkt. Ibrahim Msengi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
TU3
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika sala ya hitima ya marehemu Abdallah Rehani, baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Tabata jijini Dar es salaam Mei 17, 2015.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
TU4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim baada ya hitima ya marehemu Abdallah Rehani, baba mzazi wa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu, Tabata jijini Dar es salam Mei 17, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
TU5
Mke wa Makamu wa Rais Mama Asha Bilal akiagana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya sala ya hitima ya marehemu, Abdallah Rehani, baba mzazi wa mke wa Waziri Mkuu, mama Tunu Pinda iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Tabata jijini Dar es salam Mei 17, 2015. 

     (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: