Advertisements

Tuesday, May 26, 2015

MBIO ZA MWENGE WA UHURU UKIWA PEMBA

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Tanzania mwaka 2015/2016, Juma Khatib Chum, akimkabidhi chandarua mtoto Fatmat Abdalla Mohammed, anayeishi na VVU mara baada ya kuonyesha hali halisi ya maisha yake katika kituo cha Ushauri nasaha ZAPHA+ mkabala na ofisi ya Halmashauri ya Chake Chake Pemba.
MKUU wa Wilaya ya Mkoani isiwani Pemba Mhe:Hemed Suleiman Abdalla, akipima afya katika banda la ushauri nasaha linalomilikiwa na ZAPHA+ katika mkesha wa mwenge wa uhuru Tanzania Chake Chake Pemba.
MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Pemba Mhe:Hanuna Ibrahim Massoud, akimkabidhi Risala ya wananchi wa Chake Chake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Juma Khatib Chum, kwa lengo la Kwenda kumkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla wapili kutoka kulia, katikati ni Kiongozi wa wakimbizaji wa Mwenge wa Uhuru mwaka huu Juma Khatib Chum, akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Mhe:Hanuna Ibrahim Massoud akiwa na wakimbizaji wa mwenge wa uhuru pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Mhe:Hemed Suleiman Abdalla.
MTOTO Fatmat Abdalla Mohamed akionyesha hali halisi ya Maisha yake kwa kutumia mchoro maalimu, tokea alipoanza maisha ya kuishi kwa matumaini hadi sasa alivyo wakati wa mkesha wa Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments: