Advertisements

Sunday, May 24, 2015

Rais Kikwete atoa Msaada kwa Timu ya Kilimani Sports Club mjini Dodoma


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiikabidhi timu ya soka ya Kilimani Sports Club jezi na mipira katika ikulu ndogo ya mjini Dodoma leo asubuhi.Rais Kikwete alitoa msaada kwa timu hiyo baada ya kuwakuta vijana hao wakifanya mazoezi bila zana bora katika uwanja wa mpira ulioko eneo la Kilimani karibu na ikulu wakati Rais alipokuwa akifanya mazoezi ya kutembea katika eneo hilo.Wakiongea mara baada ya kupokea msaada huo vijana hao walimshukuru Rais Kwa moyo wake wa upendo na nia yake ya kukuza vipaji kwa vijana na kuahidi kufanya vyema katika ligi ya Wilaya ya Dodoma mjini(picha na Freddy Maro)

No comments: