Rajab Msabaha Kauzela mtia nia wa Ubunge Jimbo la Kilosa ambaye pia alikuwa Katibu Mwenezi wa Tawi a CHADEMA Washington DC
Rajab Msabaha Kauzela (wa nne kutoka kushoto) akiwa na mnadhimu wa kambi ya upinzani ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki Mh Tundu Lissu (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na viongozi wengine wa chadema Morogoro.
Rajab Msabaha Kauzela akiwahutubia wakazi wa Kilosa waliokusanyika kumsikiliza katika mkutano wa hadhara, akielezea mikakati yake endapo wana-Kilosa watampendekeza kuwamwakilishi wao katika nafasi ya Ubunge kupitia CHADEMA.
Pichani Rajab Msabaha Kauzela akiwa na Wazee wa Kilosa akiomba baraka zao ili wakubali kumpitisha kuwa mwakilishi wao katika Kinyang'anyiro cha Ubunge Jimbo la Kilosa
Wanafamilia wakimsikiliza Rajab Msabaha Kauzela alipokuwa akibadilishana nao mawazo kuwaelezea azma yake ya kutaka kugombea Ubunge Jimbo la Kilosa.
Rajab Msabaha Kauzela akiwa amepiga picha pamoja na wanafamilia siku alipokuwa anawaambia azma yake ya kutaka kugombea Ubunge Jimbo la Kilosa.







3 comments:
kumbe na chadema pia wanavunja sharia kama ccm, hawa jamaa wanadiaspora ni maraia wa nje. huyu mshikaji ni raia wa marekani sassa inakuwaje anataka kugombea ubunge wakati sio raia wa Tanzania. maana katiba yetu inasema ukichukua uraia wa nchi ingine unauvua utanzania. sasa kwa nini ccm na chadema wanaanza mchezo mchafu kama huu. halafu ona viongozi wa juu wa chadema wapo naye hapo wanakubalina na uvunjaji wa sharia. serikali inabidi iwe makini na hawa watu. juzi kati tu hapa loveness naye alionekana dododma akijiandikisha ktk daftari la kupiga kura. tunaomba serikali iwe makini na uvunjaji huu wa sharia. Tanzania hakuna uraia pacha, luka usiibanie hii ni kuelimisha na kuikoa nchi katika majanga haya ya kuvunja katiba.
Wewe anonymous hapo juu umetoka usingizini,nani kakwambia jamaa ni raia?
Mzee wa kiminyio usife moyo... endeleza sera za chadema.
Post a Comment