Advertisements

Tuesday, July 28, 2015

CHAMA CHA MAPINDUZI(CCM) KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KESHO


14 comments:

Anonymous said...

MLISHASEMA ASIYEKUBALI MATOKEO YA KAMATI KUU AHAME. SASA MKUTANO WA NINI? AU NDIO DEGEDEGE LA UKUBWANI?

Anonymous said...

Asante. Sidhani kama tutakuwa na jipya la kujitetea na wala kumlaumu Lowassa! Tuliwatuma makada wengi sana kumshambulia Lowassa na baadae kuwahonga madaraka. Kauli za NAPE nazo mchango mkubwa. Hii nini mdudu ndani ya CCM. Tupumzikeni na wala Lowassa hana makosa mimtafutie hoja..tuende kufanya uchaguzi October kwa waTanzania..

Anonymous said...

Kwa wapenzi wa CCM tunakila namna ya kujilaumu kutokana maadili mabovu na ulaji wa hali ya juu uloojitokeza humu ndani kuanzia ngazi za juu. Sasa kama chama hakina jinsi iwapo Serikaliniliyoko madarakani imeshindwa kukidhi matakwa ya waTanzania! Hivyo kuendelea kutamba kwa kushinda kishindo cha goli la mkono sio wakati wake!! Kuwatuma makada kumtukana Lowassa na kuwapa nafasi za uongozi haina maana. Tujipange upya na kumlaumu haitasaidia. Tunajua wazi wizi wa kura haukuanza leo!! Kila la heri na taarifa za Lumumba. Msisahau aliyosema mwalimu ndio imekuja wakati muafaka. Sina chama tena. Mimi nabaki mkulima wa tumbaku..

Anonymous said...

Marehemu CCM umeacha watoto na wajukuu?

Mashamba ya khana na pamba?

Wachina wa kuchoma mainyi kariakoo?

Waarabu loliondo?

Watu wa Mtwara wakipigia kelele gas yao?

Na shilling ikipaa kulinganisha na do la

Na kwa jk na mama wama wakiwa wametembea kila mahali duniani kwa kipindi kifupi cha siku 3,640 (10yrs), isipokuwa BK, Tunduma, Rombo Mashati, Arsha kwa Ngolelo, Mbalizi nk. Mungu mweke CCM mahali PePONI

Anonymous said...

ccm inasikitisha. Kauli chafu za Nape kuwa wamezuia mafuriko kwa mikono tutaona mafanikio yake. Maji yamevunja kingo zake na kujenga mkondo mwingine. Tukutane October 25, goli la mkono litadakwa mwaka huu.

Anonymous said...

he he he...asante anonymous

Marehemu CCM umeacha watoto na wajukuu Kinanana, Nape, Makamba na Mangula? Na Wasirra bado YUPOOOOOO....AWAMU ya kwanza alibakizwa na bado yupo; awamu ya PILI yupo; awamu ya tatu yupo; na awamu ya NNE? mtamwacha wASSIRRA nani jamEni???

Mashamba ya kAHAWA na pamba YAKO WAPI?

Wachina wa kuchoma maHINDI kariakoo?

Waarabu loliondo - WAMECHUKUA TEMBO WETU?

Watu wa Mtwara wakipigia kelele gas yao - MMEWAACHA WAPI?

Na shillingI YETU iMEPAA kulinganisha na dOLA

Na kwa JK na mama WA WAMA wametembea kila mahali duniani kwa kipindi kifupi cha siku 3,640 (10yrs), WAMESHINDWA TU KWENDA BUKOBA, Tunduma, Rombo Mashati, ArUSHA kwa Ngolelo, MbaliNzi MBEYAnk. Mungu mweke CCM (kama unavyoendelea kumweka KANU ya Kenya) mahali PEMA PePONI.

Anonymous said...

Natamani CCM wangemwambia Magufuli afanye haya hapa:

(a) aturudishie nyumba zetu sisi wananchi alizoziuza kwa bei sawa na bure. Hizi nyumba ni za kodi ya wananchi.

(b) pesa alizojenga nazo nyumba yake ya hekalu huko chato amezipata wapi yeye mtumishi wa sIrikali? Au ndio tuseme Chukua Chako Mapema (CCM) ndivyo mlivyo?

(c) atamsaidia vipi mama zangu na baba zangu (milioni karibu kumi) nji hii ambao wameifanyia kazi nji hii na kustaafu lakini wanapata mateso ya hali ya juu?

(d) Je pesa yote JK aliyotumia na mama watoto wake kutembelea maeneo yote huko majuu tumepata nini? Safari zake zilikuwa na Tija? Raisi wa marekani hawafanyi hivyo na pesa za walipa kodi. Kwa mfano, Mheshimiwa B.Obama amekaa katika madaraka miaka 8 (~~~siku 2,460)lakini hajatembea maili nyingi kwa mwezi mmoja kama JK wa nji maskini kama Tanzania!

(e) Bwana Booze, tuambie utaweza kuturudishia UDA yetu aliyochokua Ridhiwani?

(f) Bwana Booze utaweza pia kutuambia kwa nini tusimfunge Ridhiwani na wale wote walioangamiza reli ya kati NA YA KASKAZINI ILI MALORI YAO YAPATE BIASHARA?

Anonymous said...

Mbona mnaingia mchecheto kana kwamba mnaogopa CCM itaeleza ukweli na uozo wa lowasa hakuna wanaemjua lowasa kisiasa kama CCM kwa hivyo msijaribu kuiziba mdomo CCM kwa sababu hamtaiweza walishindwa makaburu wa South Africa

Anonymous said...

na lazima mtafutane October, nyie mnaofikiri utani subirini madiliko yanakuja.

Anonymous said...

Si msaport Lowasa lakini,ukweli ni kuwa CCM ilifanya makosa kumpa nchi JK ambae,hakufanya jitihada zozote kuimarisha chama,na kusimamamia serikali effectively.

Anonymous said...

Ccm wana ya kuongea kama vyama vyengine na pia kwa kutompa nafasi mkuu wa majambazi na mporaji ardhi maarufu lowassa ni fundisho tosha hata kwa vibaka wadogo, msahau kabisa kama ana uwezo wa kushinda. Kina slaa wanaondoka chadema wanadai wamedhalilishwa. Sasa lowassa bado anazo pesa za kununua masheikh na wachungaji wenye njaa? Au vibaka wa bodaboda? Tukutane october.

Anonymous said...

FOLKS, STOP COPYCAT MENTALITY! NANI KAWAAMBIA LOWASA NA UKAWA WATASHINDA? THAT IS SO CHILDISH KULETA USHABIKI BILA KU-ANALYZE AND DIFFERENTIATING FACTS FROM FICTIONS? HAMNA WASOMI HAPO JUU? WHERE DO YOU GUYS GET ALL THESE NONSENSE? MSIMPIGIE DEBE LOWASA, HE CANNOT BE SALVAGED WHEREVER HE GOES. WANANCHI WATAMPIGIA KULA KIONGOZI MWENYE CHARACTER NA MWAMINIFU, NA AMBAYE NI MAHIRI NA MCHAPAKAZI. PIA, KIONGOZI WHO IS LIKE THEM, SIMPLE AND OF MODEST MEANS. NOW UKIMCHUKUA DR, MAGUFULI VS LOWASA? OBVIOUSLY, MAGUFULI IS A SIMPLE MAN AND NOT VERY WEALTHY LIKE LOWASA. WATU WATAMUONA YEYE NI KAMA WAO. ALSO, AS OF THIS YEAR, MAGUFULI AMECHAPA KAZI NA KILA MKOA UMEONA INFRASTRUCTURES IMPROVED. LOWASA, LABDA WATU WA MONDULI NDIYO WAMEONA ALICHOWAFANYIA. SCANDALS OR SUSPICION OF SCANDALS? NADHANI LOWASA ANA KAZI NGUMU YA KUJIELEZA KWA WANANCHI NA RICHMOND SCANDAL, IT WILL HAUNT HIM FOREVER, NO MATTER HOW MASHABIKI WAKE WATAJARIBU KUI-TWIST! DEFINITELY, MIKOA YA ZIWA, SHINYANGA, TABORA, SINGIDA, DODOMA, RUKWA, ITAMPIGIA..MAGUFULI,KUNA MORE VOTES. ATABEBA KUSINI,NA NYANDA ZA JUU KUSINI AS WELL (ccm STRONGHOLDS). THE BEST LOWASA NA UKAWA CAN DO IS THE NORTH..ARUSHA, KILIMANJARO, MANYARA, ETC..HII NI MIKOA AMBAYO ACCORDING TO MY ANALYSIS, WADAU WOTE HAPO JUU MNAOMPIGIA DEBE LOWASA NA UKAWA MNATOKA..AU SIYO?

Anonymous said...

Haya bania na hii dj uchuro mkubwa. Huu ndio ujinga wa mtu mwenye career ya muziki kuwa na responsibility kama hii ya kuwa na final say kwenye hii blog ya vijimambo. Unashindwa kudraw the line on when to impress ubalozi wako na serikali wezi and when unatakiwa kupost comment za watu wanaopoteza muda wao kusoma na kucomment kwenye hii blog. Kabla sijakushauri kurudi shule kupata elimu ya UPE, napenda ukumbuke kwamba penye ukweli UWONGO hujitenga na hata usipopost comments setu tutasiweka pengine. dj mwenyewe just uchuro.

Anonymous said...

Wewe ananymous July 29, saa 5:15 a.m. unapiga nani kelele, wewe nani. Ongea kiistaarabu tafadhali. Huna a kili hata Chem be ya kuchanganua mambo, uko sawa na baba na mama yako, marehemu Ccm...enendeni mkarehemiwe kwa amani. Hata siku yes atakaporudi, sidhani kama ataweza kubeba laana zote zilizofanywa na chama cha mihuni mihuni tu a kina nape, makonda, msekwa na kina makamba. Poleni sana kwani kama una uelewa kidogo tu, kumbuka kwamba hata Gobachev alishindwa kuzuia mabadiliko!