Advertisements

Thursday, July 2, 2015

Rais Kikwete na Waziri Mkuu wa Ethiopia wazindua kiwanda cha Kudhibiti Malaria Pwani


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuzindua rasmi kiwanda cha kuzalisha viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza Malaria kilichopo eneo la viwanda TAMCO kibaha,Mkoani Pwani leo.Kulia ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia wakiangalia uzalishaji wa viuadudu vya mbu wanaoeneza Malaria kilichopo eneo la viwanda TAMCO kibaha,Mkoani Pwani leo muda mfupi baada ya uzinduzi rasmi leo.
 


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn muda mfupi kabla uzinduzi wa kiwanda cha kudhibiti malaria Mkoani Pwani leo.
(picha na Freddy Maro). 

No comments: