Kiwanda cha Sukari cha Kagera tayari kilishaanza
kuzalisha ziada ya sukari inayohitajika katika soko la sukari Nchini
hali inayopelekea kuweza kupunguza tatizo la upatikanaji wa sukari
Tanzania na Nchi za jirani zinazotumia sukari kutoka kiwandani hapo.
Kiwanda
hicho cha Sukari cha Kagera kiko katika sehemu Kaskazini Magharibi ya
Tanzania (karibu na mpaka wa Tanzania na Uganda) kilibinafsishwa na
Serikali kwa sekta binafsi mwaka 2001. Malengo ya ubinafsishaji yalikuwa
kuboresha upanuzi wa masoko ya ndani na kikanda, uwekezaji wa kisasa,
upanuzi na ukarabati na majengo ili kuhakikisha shughuli za kiundeshaji
zinaboreshwa.
Mto wa Kagera ni kati ya mito inayounda mto wa Nile pia ni mto mkubwa kabisa wa kuingia ziwa la Viktoria Nyanza.
Inaanza Burundi inapounganika mito ya Nyawarongo na Ruvuvu ikiendela 400 km hadi kuingia ziwa la Victoria Nyanza.
Mto
wa Kagera ukielekea kaskazini ni mpaka kati ya Tanzania na Rwanda; pale
inapogeuka kuelekea mashariki karibu na mji wa Kikagati ni mpaka kati
ya Tanzania na Uganda. Sehemu ya mwisho wa njia yake inaingia kabisa
ndani ya eneo la Tanzania hadi kufika Viktoria Nyanza kama 40 km
kaskazini za Bukoba. Jina la Mto wa Kagera umekuwa pia jina la mbuga
ya wanyama ya Akagera National Park huko Rwanda na pia la Mkoa wa
Kagera katika Tanzania.
Wakiingia Eneo la lango kuu la Kiwanda hicho cha Kagera Sugar. Mbele ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo
Wanafunzi hao waliongozwa na Walimu wao katika Ziara hiyo
Wanafunzi
wakipata kuonja sukari hiyo inayopatika hapo kiwandani baada ya
kujionea tangu Miwa inatoka shambani mpaka uundwaji wake!
Bw. Moses Mwanga akiwa ndani ya Maabara ya Kiwanda hicho akitoa maelezo kwa Wanafunzi, Habari na Picha na Faustine Ruta, Bukoba
No comments:
Post a Comment