Advertisements

Wednesday, August 5, 2015

BREAKING NEWS: MKUTANO WA PROF. LIPUMBA WAHAIRISHWA BAADA YA WANACHAMA KUZINGIRA OFISI YA CHAMA HICHO

Ilikuwa leo Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim azungumze na Wanahabari asubuhi hii ila mkutano huo umehairishwa hadi siku nyingine tena. Wananchi wa chama cha wananchi CUF wamezingira ofisi za chama hicho wakiongozwa na wazee wakitaka kujua hatima ya wenyekiti wao Prof.Ibrahim Lipumba aliyedawai kutaka kujiuzulu.
Magdalena Sakaya ameulizwa Prof. Lipumba alitaka kuzungumza nini na akajibu wao hawajui kitu alichotaka kuwaambia wananchi Sababu kubwa ya kusitishwa mkutano, Magdalena amesema Wazee wa CUF wametaka kujua kwanza ni kitu gani Mwenyekiti anataka kuongea Wananchi nje ya ofisi za CUF wanashangilia wakiimba kwa kusema 'Si mnaona, muziki wa Lipumba kuuzima hamuwezi'


Mmoja wa Wananchi wanaoshangilia amesema wamefurahia kwakuwa wanaamini Mwenyekiti wao Lipumba hajiuzulu na yuko na wananchi. Wananchi tofauti wanaoshangilia wanasema wanamuamini Lipumba na dalili iliyopo ni kuwa hawezi jiuzulu maana anawasikiliza na ataendelea kuwa Mwenyekiti daima

1 comment:

Anonymous said...

chihendo na mwenye mwana.maana yake shughuli na mwenye mwana na mwenye mwana ni ccm.kazi kweli si mchezo.mwenye akili atafakari sana kauli hii iliyotolewa na mkuluu.

nchii hii ni ccm inataka kushika dola kila siku hakuna kingine wala zaidi ya kingine.

tizama mipasuko wanavyojaribu kupasua katika vyama vya upinzani wenyewe kwa wenyewe wanagombana.wameshapenyezewa RUPIA kwisha kabisa.penye uzia penyeza rupia.

tizama kule alivyoingia kigongo makapi kapi ya ccm wasio na fikra wataona amewaongezea nguvu kumbe amakuja kukivunja.KHERI YA DR SLAA anaye ona mbali hata mkimkebehii.

mreham alivyoanzisha nccr mageuzi kipo wapi sasa.wamefukuzwa ccm wote halafu mnawapokea kisa kuongeza nguvu hujui kama WAMETUMWA KUJAA KUKIBOMOA BOMOA CHAMA.MNAWAKOPKEA TUU.NA cuf huko visiwani.

mtu anakujana kusema mapinduzi oyeeeeeeeeeee mapinduzi damaima.

una wazimu.watu wameuliwa wazazi,ndugu jamaa na watoto wao bila sababu zozote kwa propaganda halafu mtu mnampokea na kukimbisheni mapinduzi oyeeeeeeeeeee mapinduzi daima.