Advertisements

Sunday, August 30, 2015

UCHAGUZI WA MWAKA HUU TANZANIA HAUNA MDAHALO WA UGOMBEA NAFASI YA RAIS?

Nimekuwa nikifuatilia taarifa mbalimbali kuhusu uchaguzi utakao fanyika tarehe 25 October lakini sijasikia tetesi kama kutakuwa na mdahalo wa ugombea nafasi ya urais. Inawezekana upo lakini mimi sijasikia na kama ni hivyo basi wanaohusika kuuandaa wahabarishe wananchi.

Huu mdahalo unahitajika sana ili tuweze kuwajua vizuri hawa wanaotaka kuwa viongozi wetu. Wagombea wote wa vyama vinavyo shiriki wakutanishwe waulizwe maswali ya msingi (live) tuweze kupima majibu na uwezo wao. Midahalo ni imekuwa inapewa umuhimu mkubwa sana kwa nchi za wenzetu. Yawezekana kuna ambao wana sera nzuri lakini hatujapata nafasi ya kuwasikiliza. Uwezo wa kujieleza kwa kiongozi ni kitu muhimu sana. Pamoja na kwamba ahadi zinazo tolewa majukwaani huwa hazitimizwi zote, na hili siyo Tanzania tu bali hata nchi zilizo endelea; lakini pale mtu anapotamka anakuwa recorded. Mtu anaye kaa kimya ni ngumu kumwelewa na hutaweza kumhoji kwa kile ambacho hakutwambia au kuahidi.

MDAHALO UITISHWE

2 comments:

James Bond said...

Hahaha nafikiri ndugu yangu huna history nzuri ya CCM ..CCM ni mwiko mgombea wao kuingia kwenye mdahalo..hilo halina mjadala:( ndiyo maana ni lazima tuwatoe hawa majambazi kama kweli tunahitaji demokrasia ya kweli Tanzania. .

Anonymous said...

Midahalo ipo uchaguzi wa mwaka huu. Subiri tutahabarishwa wakati muafaka ukifika.