Advertisements

Saturday, September 5, 2015

LOWASSA ALIVYOUTIKISA MJI WA TABORA LEO

 Aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mngeja akiuhutubia Umati wa wakazi wa Mji wa Tabora, waliofutirika kwa wingi kwenye Uwanja wa Town School, kulikofantika Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, leo Septemba 5, 2015.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika mwamvuli wa Ukawa kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila, akilakiwa kwa shangwe na wananchi wa mji wa Tabora, wakati akipita kuelekea jumwaa kuu, wakati wa Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, leo Septemba 5, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Fredrick Sumaye akisalimiana na Mke wa Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa, wakati alipowasini kwenye Uwanja wa Town School, kuhudhulia Mkutano wa Kampeni, leo Septemba 5, 2015.
Umati wa wananchi wa Mji wa Tabora ukiwa kwenye Mkutano huo.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini katika mwamvuli wa Ukawa kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila, akimwaga cheche zake katika Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, leo Septemba 5, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Fredrick Sumaye, akisisitiza jambo katika Mkutano wa Kampeni za kunadi sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, leo Septemba 5, 2015.
Chopa iliyompakia Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, ikipiga misele juu ya uwanja wa Mkutano, leo Septemba 5, 2015, mjini Tabora.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akipanda jukwaani kwa kukimbia mara baada ya kutua na Chopa yake, leo Septemba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwasalimia wananchi wa Mji wa Tabora, leo Septemba 5, 2015.
Meza Kuu.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe akiwasalimia wananchi wa Tabora.
"Mabadilikooooooo......"
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia na kunadi sera zake kwa wananchi wa Mji wa Tabora, wakati wa Mkutano wake wa Kampeni uliofanyika leo Septemba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa wakicheza sambamba na wananchi wa Tabora, waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Town School, mjini humo leo Septemba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na Mwenyekiti wake, Mh. Freeman Mbowe, wakati wakitoka kwenye Mkutano wa hadhara wa Kampeni, Mjini Tabora leo Septemba 5, 2015.


4 comments:

Anonymous said...

Na bado ukawa nawapenda

Anonymous said...

Peoples power
Tumechoka Na CCM
Karibu Ukawa

Anonymous said...

Ahadi zimekuwa nyingi kupindukia na hazitekelezeki mbona mnatununua kwa ahadi ya mapesa kama yale ya ESCROW. Tutaendelea kulala njaa. Sukari bei sh 2500 kilo. maharage yale yanayotoka kwa mkulima cheki bei sina la kukuambia. Tandale hatuendi.!!kazi kubwa kuelekea mabadiliko.

Anonymous said...

Is Tanzania no man's land? Katika mataifa yanayojitambua sijapata kuona wala kusikia mtu mwenye kashifa ya ufisadi anaomba ridhaa ya wananchi kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Huyu fisadi akishinda uchaguzi, kweli Watanzania kwa ujumla wetu tutakuwa tumejidhihirisha kwamba hatujitambui na taifa letu litaendelea kuwa backward daima. Kwingineko, tumeona viongozi wengi wakimwaga unga wao kwa kashifa kama za uzinzi, lakini kwetu kashifa ya ufisadi inaonekana karibu sawa na kosa la kutotii maelekezo ya speaker bungeni. Ni aibu iliyoje hii?