Advertisements

Wednesday, September 2, 2015

MWIGULU HAKAMATIKI KATIKA KUINADI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI,AWALIPUA UKAWA

Mwigulu Nchemba akiwasili eneo la Mkutano nje kidogo na Mji wa Babati hii leo alipofika kwaajili ya Mkutano wa kampeni wa kuinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2015.Pia kuwanadi wagombea Udiwani na Ubunge kwa Babati Mjini.Kutoka Kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Manyara Ndg.Ndekubali,Katikani ni Mwigulu Nchemba na Mwisho kulia ni Mh.Chambili ambaye ni Mgombea Ubunge Jimbo la Babati Mjini.Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa Babati hii leo,Katika hotuba yake amesisitiza Wananchi
waachane na maigizo yanayofanywa na baadhi ya wagombea Urais bali waamue moja la Kuchagua Rais Mchapa Kazi,.Mweigulu amesisitiza Zaidi kuwa rekodi za wagombea Urais zipo wazi kila kona na kwa rika zote.Hivyo watanzania watumie fursa hii kuhakikisha Taifa linapata kiongozi Mchapa kazi ambaye ni J.Pombe Magufuli wa CCM.Sehemu ya mamia ya Wananchi waliofika kusikiliza Ilani ya chama cha Mapinduzi wakishangilia namna Ilani ya chama hicho ilivyoweka bayana namna ya Kutekekeleza shughuli za maendeleo katika Jimbo la Babati Mjini,Mh.Mwigulu Nchemba akiwa na Mgombea Ubunge Jimbo la Babati Mjini Ndg.chambili wakiagana na Wananchi mara baada ya Mkutano huo wa kampeni wa CCM."CCM ni Ile Ile"
Picha na Sanga Jr.

2 comments:

Anonymous said...

Mwigulu chapuo la CCM kula kwa mbele chezea tu.

Anonymous said...

Kwani shida nini ni UKAWA tuu, hakuna vyama vinginevyo. Hii inadhihirisha uoga wa wazi kabisa na kwa misingi hii ni kuendelea kumpa huyu UKAWA kujulikana zaidi. Yaani anatangazwa mno mbona hatumsikii TLP au CHAUMA?? Kuna nini huko UKAWA?? Mmnatuchosha kwani kila mkutano Ukawa EL. Amekuwa pilipili kuwasha. Sera zimetuchosha ni yaleyale Mwigulu wangu.