Mchezo wa hatua ya pili kuwania kufuzu kwa
Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi kati ya
Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Algeria (The Fox Desert) utafanyika tarehe 14
Novemba, 2015 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kikosi cha Stars chini
ya Kocha Mkuu Charles Mkwasa kimefanikiwa kusonga hatua ya pili ya michuano
hiyo baada ya kuiondosha Malawi (The Flames) kwa jumla ya mabao 2-1, nyumbani
ikishinda 2-0, na kufungwa 1 – 0 jijini Blantyre.
No comments:
Post a Comment