Mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd, Salim
Asas Abri (aliyesimama) akitoa maelezo ya kiwanda cha kuzalisha maziwa
na bidhaa zake kilichopo mkoani Iringa kwa Waziri wa Maendeleo ya
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Titus Kamani wakati ya ziara ya kutembelea
nyanda za juu kusini kupitia mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa
afrika ya mashariki awamu ya pili.
Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa Afrika Mashariki (East Africa Dairy Development) ni mradi wa miaka mitano (2013-2018) unatekelezwa kwa awamu ya pili katika nchi za Kenya, Uganda na Tanzania kwa mfumo wa kitovu cha maziwa (dairy hub).
Nchini Tanzania mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambao unatekelezwa kwa ubia-kongano (consortium partnership) kati ya Heifer International (msimamizi mkuu wa mradi na kuongoza uzalishaji maziwa) kwa kushirikiana na Technoserve (biashara na masoko ya maziwa).
Mitamba katika shamba la Kibebe linalomilikiwa na
Richard Phillips lillilopo karibu na kijiji cha Tagamenda
wilayani iringa.
Nyati maji (water buffaloes)
katika shamba la Asas Dairy Ltd lililopo karibu na kijiji cha
Igingilani wilaya ya Iringa Waziri wa maenedeleo ya mifugo pia
alitembelea katika ziara yake.
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Mhe Dkt Titus Kamani (kushoto) akibadilishana mawazo
na Afisa mifugo Manispaa
ya Iringa Dr. Augustino Nyenza.
Afisa mifugo Manispaa ya Iringa Dr.
Augustino Nyenza (wa pili kushoto) akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi
machinjio ya kisasa yalipo Ngelewale kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe
Dkt Titus Kamani wakati ya ziara ya kutembelea Nyanda za Juu Kusini
(southern highlands) kupitia mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa
afrika ya mashariki awamu ya pili.
Mkurugenzi wa Kibebe Farms Richard
Phillips (katikati)akitoa salamu kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe
Dkt Titus Kamani wakati ya ziara ya waziri huyo.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa (katikati)
Amina Masenza akitoa taarifa ya maendeleo ya sekta ya mifugo
kwa aziri wa Maendeleo ya
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Titus Kamani (wa pili kushoto) wakati ya ziara
ya waziri huyo iliyoratibiwa na Mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki (East
Africa Dairy Development). (PICHA ZOTE NA FRIDAY
SIMBAYA)
No comments:
Post a Comment