Advertisements

Wednesday, October 14, 2015

MWILI WA MAREHEMU DK KIGODA WAPOKELEWA JIJINI DAR

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akizungumza na vyombo vya habari jinsi alivyomfahamu aliyekuwa waziri wa Viwanda na Biashara, marehemu Dk Abdallah Kigoda wakati wa mapokezi ya mwili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam jioni hii, ukitokea India ambako alipatwa na mauti.
 Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, na Mgombea ubunge Jimbo la Handeni kupitia CCM, marahemu Dk Abdallah Kigoda, ukihamishiwa kwenye gari lingine wakati wa mapokezi ya mwili huo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana, ukitokea nchini India ambako alipatwa na mauti. Mwili huo ulikwenda kuhifadhiwa Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, kusubiri kuagwa kesho katika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam
 Dk Magufuli akimfariji mtoto wa marehemu Dk Kigoda kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam
 Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha Rose Migiro akimfariji dada  yake na marehemu Dk Kigoda, Dk Aisha Kigoda.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza akimfariji mjane wa marehemu Dk Kigoda, Rasul Kigoda
 Dk Magufuli akizungumza jambo na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue wakati wa mapokezi ya mwili wa marehemu Dk Kigoda Uwanja wa Ndege.
 Dk Magufuli akisalimiana na wananchi waliofika kuupokea mwili wa marehemu Dk Kigoda
Dk Magufuli (kulia) akiangalia jeneza lenye mwili wa Dk Kigoda ukishushwa wakati wa mapokezi ya mwili huo kwenye Uwanja wa Ndege, Dar..PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

1 comment:

Anonymous said...

Tunatoa pole kwa familia na WaTanzania kwa kuondokewa na kipenzi chetu tulivu na mchapakazi. Tumsindikize kwa amani na upendo bila kuweka Kampeni za kisiasa kama zilozofanyika hiko Same Kisumo! WaTanzania ni wamoja hasa inapofikia mahali pa tukio kama hili ni mwenzetu haijalishi itikadi za vyama. Amani.