Advertisements

Sunday, November 29, 2015

KOCHA SUPER D AMNOWA BONDIA IBRAHIMU CLASS KING CLASS MAWE

Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimfanyisha mazoezi ya nguvu na kujenga misuli bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mpambano wake na Twaha Kassimu utakaofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Morogoro desemba 25 
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' akifundishwa jinsi ya kupiga ngumi za mkunjo wa chini 'UpCat' wakati wa mazoezi ya bondia huyo kujiandaa na mpambano wake na Twaha Kassimu utakaofanyika Desemba 25 katika uwanja wa jamuhuri morogoro
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' juu akimfanyisha mazoezi ya misuli ya shingo kupandisha na kushusha shingo uku akiwa juu ya bondia Ibrahimu Class 'King class Mawe' wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mapambano ya kitaifa na kimataifa ya bondia huyo 

Na Mwandishi Wetu
KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amendelea kuwamwagia sumu mabondia Ibrahimu Class 'king Class Mawe' na Vicent Mbilinyi wakati wa mazoezi yao ya kujiandaa na mapambano yao yatakayofanyika desemba 25 katika uwanja wa jamuhuri Morogoro

wakati Class akimvaa Twaha Kassimu bondia vicent Mbilinyi atavaana na bondia mkongwe kabisa Deo Njiku wa Morogoro

akizungumzia mazoezi ambayo anampa bondia bigwa wa mikanda miwili ya U.B.O na WPBF Afrika Ibrahimu Class ambapo kwa sasa anamfanyisha mazoezi ya kumjengea nguvu pamoja na akili kwa ajili ya mchezo wake ujao

ambapo amekuwa akimfanyisha mazoezi mbalimbali ya nguvu yakiwemo ya kujenga misuli ya tumbo pamoja na shingo ambapo bondia huyo kwa sasa anafanya mazoezi mara tatu kwa siku na kusimamiwa vizuri

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile

Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

No comments: