Thursday, December 10, 2015

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR, BALOZI SEIF ASIMAMISHA UJENZI WA NYUMBA YA GHOROFA MJINI UNGUJA, ZANZIBAR

Balozi Seif akipokea malalamiko ya Wakaazi wa Mtaa wa Mlandege wakimshutumu Mmiliki wa Kiwanja cha jengo la Ghorofa Bwana Anuari Abdulla anayejenga pamoja na eneo la wazi. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwasili mtaa wa Mlandege kukagua kiwanja cha nyumba ya Ghorofa kinacholalamikiwa na Wakaazi wa Mtaa huo kwamba kimevamia pia eneo la wazi linalotumika kwa shughuli za Kijamii.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwasili mtaa wa Mlandege kukagua kiwanja cha nyumba ya Ghorofa kinacholalamikiwa na Wakaazi wa Mtaa huo kwamba kimevamia pia eneo la wazi linalotumika kwa shughuli za Kijamii.
Mmiliki wa Kiwanja cha nyumba ya Ghorofa Mlandege Bwana Anuari Abdullah akijitetea kupata kibali kinachomruhusu kuendeleza ujenzi wa nyumba yake.
Mmiliki wa Kiwanja cha nyumba ya Ghorofa Mlandege Bwana Anuari Abdullah akijitetea kupata kibali kinachomruhusu kuendeleza ujenzi wa nyumba yake.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amemuagiza Mmiliki wa Kiwanja kinachotaka kujengwa Nyumba ya Ghorofa katika Mtaa wa Mlandege Bwana Anuari Abdulla kusitisha mara moja ujenzi huo.
Mmiliki wa Kiwanja cha nyumba ya Ghorofa Mlandege Bwana Anuari Abdullah akifanyiwa mahojiano.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiondoka eneo la tukio mara baada ya kutoa maamuzi ya kuzuia ujenzi wa jengo la Ghorofa kwa kukosa taratibu zinazozingatia Mji mkongwe wa Zanzibar. PICHA/VIDEO NA CATHBERT KAJUNA WA KAJUNASON BLOG.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amemuagiza Mmiliki wa Kiwanja kinachotaka kujengwa Nyumba ya Ghorofa katika Mtaa wa Mlandege Bwana Anuari Abdulla kusitisha mara moja ujenzi huo. Hatua hiyo ya Balozi Seif imekuja kufuatia malalamiko makubwa yaliyotolewa na wakaazi wa Mtaa huo wakimshutumu Mmiliki huyo kuvamia pia eneo la wazi (Open Space) la shughuli za kijamii katika sehemu hiyo. Balozi Seif alimuonya Mmiliki huyo kwamba endapo ataendelea kukaidi agizo alilopewa na Mamlaka Nne zinazosimamia na kushughulikia masuala ya Ujenzi Serikali italazimika kumchulia hatua za kisheria dhidi yake.
 “ Tumebaini kwamba unaendelea kwenda kinyume na maamuzi uliyopewa ya kusitisha ujenzi wa Jengo lako. Sasa endapo utaendelea kufanya hivyo Serikali italazimika kukuchukulia hatua za kisheria zinazofaa “.
 Alisema Balozi Seif. Alifahamisha kwamba wakaazi wa Mtaa wa Mlandege ambao wanaishi ndani ya eneo la Mji Mkongwe lililopata hadhi ya kuwa Urithi wa Kimataifa wanapaswa kuzingatia matakwa yaliyokubalika katika uhifadhi wa Mji huo wa Kihistoria. Mapema Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe wa Zanzibar Nd. Issa Sarboko Makarani alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Mmiliki wa kiwanja hicho amekuwa akikaidi maamuzi anayopewa kuyatekeleza na mamlaka husika katika ujenzi huo.
 Nd. Sarboko alisema Bwana Anuari ameamua kuendeleza ujenzi huo kwa kutumia kibali alichopewa na Mmoja wa Afisa wa Baraza la Manispaa ambacho tayari kimeshafutwa kwa vile kinakiuka na kutozingatia sheria na taratibu zilizowekwa. Alisisitiza kwamba Mmiliki huyo tayari ameshaonywa na Viongozi wa Taasisi Nne waliokutana kujadili suala hilo na kumtaka asubiri maamuzi ya pamoja yatakayotolewa baada ya kuzingatia hali halisi ya namna yatakavyozingatia matakwa na haki ya kila upande unaohusika. “ Kibali cha Ujenzi wa Jengo hili kinachodaiwa kutolewa na Baraza la Manispaa Zanzibar kimefutwa kwa pamoja na wakurugenzi Wanne wa Idara za Ardhi, Mamlaka ya Mji Mkongwe, Baraza la Manispaa pamoja na Idara ya Ujenzi na Mipango Miji “. 
Alifafanua Nd. Sarboko. Alimtaka Mmiliki huyo kuhakikisha kwamba mabati yaliyowekwa kufunga eneo la wazi lililokuwa likitumika kwa wapita njia pamoja na kutumika kwa shughuli za Kijamii anayaondoa mara moja vyenginevyo watendaji wa Mamlaka hiyo watalazimika kutekeleza amri hiyo kwa kutumia kijiko katika kipindi kifupi kijacho.

2 comments:

Anonymous said...

Habari nzuri hiii ila kwa mtizamo wa kufikiri na kuelewa haya mambo hayakuanza leo hii baada ya mhe. Rais DR. Magufuli kuonyesha kuwa anataka uwajibikaji sio lelemama! Viongozi hawa hawa walikuwepo na hakuna lililofuatiliwa kuona haki ipo, na ndio maana hata swala la ESCROW ni kitendawili kikubwa! walikuwa na uwezo wa kukemea maovu na haki kuporwa lakini ukimya ulitawala ilani ya chama hakkuna kusemana au kuchukuliana hatua. Ilala hospital wailkuwa wanachaji x-ray tsh. 15000/ sasa hivi wameshusha elfu tatu tuu!! Hizo za juu walizokuwa wanavuna zilikuwa zinaenda wapi tuyapate majibu yake?!! Sasa basi kama ni nyumba zinazojengwa kusikohusika ziko nyingi sana, rejesheni hivyoo viwanja vya kuchezea..

Anonymous said...

Nchi hii ya ajabu sana,Does it take a vice president kwenda kusimamisha ujenzi au kuunganisha maji! Mamlaka ziko wapi?