Advertisements

Thursday, February 4, 2016

HABARI NJEMA "LADY IN RED" KUFANYIKA UINGEREZA 13/FEB/2016

Lady In Red ni onesho la mitindo ambalo limekuwa likifanyika kwa muda mrefu hapa nchini Tanzania, Onesho hilo lilianzishwa na Mama mitindo maarufu nchini kama Asya Idarous, kwa lengo la kuendeleza na kuibua vipaji vipya ndani ya Tasnia hiyo ya Mitindo. Kadri siku zinavyo zidi kusonga Onesho hilo limeendelea kuwa na ufanisi mzuri ukilinganisha na awali, ikiwa ni pamoja na ongezeko la hamasa kwa wanamitindo na kuwapa muamko wa kimaendeleo zaidi kupitia Onesho hilo, hasa kwa kuwapa kipaumbele upcoming Designers.


Lady In Red 2016 kwa sasa inaelekea kuwa ya kimataifa kufuatia hamasa kubwa ya Onesho hilo kwenda kufanyika nchini Uingereza. Hii ni habari njema kwa wote wapenzi wa mitindo yaani designers, models na wadau wengine.

Lady In Red 2016 Tanzania imefanyika 31/1/2016 katika ukumbi wa Danken House Jijini Dar, ambapo ilifanikiwa kung'ara kwa style yake, chini ya usimamizi mzuri kabisa wa Asya Idarous, siku hiyo ndipo ilitangazwa Rasmi kuwa Lady In Red 2016 kwa mara nyingine itafanyika nchini Uingereza usiku wa kuamkia valentine day tarehe 13,/2/2016. Siku hiyo nyota wa wimbo wa "Pacha wangu" maarufu kama Rich Mavoko, akitokea hapa Tanzania atatumbiza kwenye onesho hilo. Support yako inaweza ikapelekea Lady In Red iwe yakimataifa zaidi.

Maelezo By Victor Petro

No comments: