Ndugu
zetu pamoja na Marafiki zetu, wakati huu tukiendelea kuomboleza msiba
wa mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga, tunapenda kutoa shukrani za dhati
kwa ushiriki wenu wa hali na mali katika kuandaa safari yake ya mwisho.
Katika
kumuenzi na kukumbuka urafiki wake wa kipekee, Kamati ya Maandalizi ya
Dar es Salaam inawaalika na kuwakaribisha katika kusanyiko la kumuenzi
jioni ya tarehe 30 April 2016 kuanzia saa 11 jioni pale Triple 7 (@777).
Kusanyiko hili ni mahsusi kwa mambo mawili makubwa, moja likiwa ni
kukumbuka na kuenzi maisha yake katikati yetu na pili kupashana habari
za kuhitimisha maandalizi ya Safari ya kumuweka katika nyumba yake ya
Milele.
Naomba tujumuike wote na tunaamini hata huko aliko atafurahi tunapomkumbuka.
Bwana ametoa na Bwana Ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe
Imetolewa na Dr. George Longopa
KNY Kamati ya Maandalizi ya Dar Es Salaam
Simu 0754 870969
2 comments:
kweli inaonyesha ni namna gani alikuwa ni mtu wa watu,mi nilijua ni US kumbe mpaka nyumbani TZ wanamuandalia...hata hao wanaokaa nakusambaza kwenye mitandao maneno yakumchafua marehemu kwamba alikuwa hivi na vile wewe ni msafi vipi unayemuhukumu mwenzako ,nadhani sasa aibu zenu jinsi watu walivyo hawajayaona hayo mnayoyaongea kijana mdogo mazishi yake utadhani alikuwa kiongozi fulani wa nchi kisa roho yake ilivyokuwa nzuri kwa wenzake yaani kwa ujumla ni mtu wa watu...R.I.P KING ANDREW
He was a true definition of a full of life. May your soul rest in peace Friend. You are truly missed.
Post a Comment