Advertisements

Thursday, May 26, 2016

Mayunga aeleza kwanini aliamua kuvunja mkataba na Universal Music1

Mayunga asema kwa sasa ana nafasi ya kufanya hata albamu na Akon
Msanii wa muziki wa Tanzania aliyefanya kazi na Akon baada ya kushinda shindano la Airtel Trace Music, Mayunga amesema nafasi ya kukutana na Akon na kufanya naye kazi imemhakikishia nafasi ya kufanya kazi nyingi zaidi.
Akizungumza na Bongo5 Jumatatu hii, Mayumba amesema amejihakikishia nafasi ya kufanya hata albamu na msanii huyo mahiri kutoka Marekani.

“Nataka kushare na watanzania wasije wakaona Akon ndiyo basi tena, sijui nimeichezea bahati kwa Akon, labda ningemuacha na Akon aweke mistari yake mule no. Niseme tu kwamba na uwezo wa kufanya ngoma na Akon zaidi ya mbili, tatu, nne hata albamu naweza. Na hiki ni kitu ambacho nilikuwa nataka mimi, kwamba nikukutana na Akon lazima nitegeneza mahusiano ya kazi nyingine,” alisema Mayunga.

No comments: