Advertisements

Monday, May 23, 2016

MKENYA AFUNGA NDOA NA MWANAMME MWENZAKE MICHIGAN, NCHINI MAREKANI

Bw. Ben Gitau na Bw. Steve Damelin

KATIKA matukio ambayo wanaume wa Kenya wanaoana na wanaume wenzao katika nchi zinazoruhusu jambo hilo, mwanamme mmoja wa Nakuru, Kenya, amefunga ndoa na profesa wa hisabati wa Marekani.

Bw. Ben Gitau (33) na Bw. Steve Damelin walioana wiki iliyopita huko Ann Arbor, Michigan, Marekani, Jumamosi alasiri ambapo baada ya tukio hilo wawili hao walionekana wakibusiana na kukumbatiana ambapo marafiki na wanafamilia walipiga vigelegele na kushangilia.

Hata hivyo, mshauri mmoja wa masuala ya kifamilia , Mchungaji Philip Kitoto wa International Christian Centre, Nairobi,alilaani ndoa hiyo akisema: “Kiutamaduni na kwa mujibu wa Bibilia, ndoa na kujamiiana kati ya watu wa jinsia moja ni dhambi.”


“Biblia iko wazi kwamba Mungu alituumba kwa taswira yake; mme na mke. Katika kitabu cha Mambo ya Walawi 18:22 Mungu anamwonya mwanaume kutofanya ngono na mwanaume mwenzake kama anavyofanya na mwanamke.”

Bw. Kararu Ririe, rafiki wa karibu wa wanandoa huyo ambaye ni Mkenya aliyewahi kukiri kwamba ni shoga anayeishi California, Marekani, alitume ujumbe kwenye mtandao wa twitter baada ya ndoa hiyo akiandika kwamba: “Jioni hii nilimpongeza rafiki yangu, Ben na mumewe Steve, kwa ndoa yao. Ni jambo adimu kwa Mkenya kuwa jasiri kiasi hicho. Hongera.”

Gitau alikuwa anaishi Atlanta, Georgia, kabla ya kuhamia California. Kwa mujibu wa mwanafamilia mmoja aliyezungumza na gazeti la Daily Nation, Gitau alikutana na mchumba wake huko Atlanta ambako Damelin alikuwa mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD) katika Chuo cha Teknolojia cha Georgia.

Katika kulaani tukio hilo, Mchungaji Kitoto alisisitiza kwamba tendo la ndoa kati ya mwanamme na mwanamke liliwekwa kwa ajili ya uzazi.

Ndoa za jinsia moja zilihalalishwa katika Jimbo la Michigan mwaka jana mwezi Julai na Mahakama Kuu ya Marekani iliyoondoa sheria zinazopinga ndoa za watu wa jinsia moja mradi tu wawe wanapendana




DAILY NATION

2 comments:

Anonymous said...

Hebu tuache unafiki. Tusisahau Misahafu inaruksa ya kukataza ushoga. Hilo tuwaaachie waumini. Lakini iwapo watu wawili wanataka kufanza hivo basi tuwaaachie ili mradi hawakai kwako ama kuingilia mambo yako. Hili ni lao baina yao! Sisi sote tunafahamu miaka yote hawa jamaa wapo na tulikuwa tunawaita wasenge ama mabasha! Wapo Dar, Zanzibar etc. Tupende tusipende hayazuiliki miaka inavyoongezeka.

Anonymous said...

Eh Mungu baba tusaidie