22/05/16 Mkuu wilaya ya Iringa Mh. Richard Kasesela alitembelea maduka ya vijana wajasiliamali walifungua maduka ili kuweza kunyanyua maisha yao. vijana hawa wamepata mikopo na kuweka maduka yao katika hadhi ya kimataifa. Akizungumza nao Kasesela alifurahishwa sana na unadhifu wa maduka hayo yaliyopo mtaa wa msikiti wa miyomboni. Kasesela hutumia jumapili kutembelea wafanya biashara ndogondogo na wale wa sokoni ili kuwahamasisha kukuza biashara zao na kuitangaza. Maduka haya yana wiki moja tu tu toka yaanzishwe hayana tofauti na yale ambayo ukienda nje ya nchi utayakuta. Wajasilia mali walialamikia wingi wa kodi ndogo ndogo pia mazingira ya baishara bado si rafiki sana. Mkuu wa wilaya aliahaidi kulifanyia kazi.
ALITEMBELEA maduka ya fettilicious, M8, Young D na mengineyo.
Mh. Richard Kasesela akiwa kwenye moja ya maduka hayo
No comments:
Post a Comment