Advertisements

Thursday, May 26, 2016

YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA



Kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kikiendelea leo mjini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Ackson akifuatilia kwa makini michango ya wabunge wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu ndani ya Bunge mjini Dodoma.


Waziri wa Elimu,Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako akijadiliana jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde bungeni mjini Dodoma.

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka 20016/2017 mjini Dodoma. Wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2016/2017 imeomba kupitishiwa shilingi Trilioni 1.39 . 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angella Kairuki akifuatilia jambo ndani ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo. 

Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo.Picha/Aron Msigwa-MAELEZO.

No comments: