Saturday, June 4, 2016

MUHAMMAD ALI AFARIKI DUNIA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 74

Muhammad Ali enzi za uhai wake.

Bondia bingwa wa zamani wa dunia, Muhammad Ali ‘The Greatest’ amefariki dunia jana Ijumaa akiwa kwenye Hospitali ya Phoniex alipokuwa akitibiwa tatizo la mapafu. Muhammad amefariki akiwa na umri wa miaka 74.
Akiwa na watoto wake, Laila (kushoto) na Hana (kulia)

Muhammad alifikishwa kwenye Hospitali ya Phoniex iliyopo Jimbo la Arizona juzi Alhamisi baada ya kuzidiwa huku akiwa anapumua kwa shida na kikohozi kikali cha mara kwa mara. Mbali na tatizo la mapafu, Muhammad amekuwa akisumbuliwa na tatizo lingine kubwa zaidi kwenye mfumo wa fahamu ‘nervous system’ ambalo kitaalam linajulikana kama Parkinson.

Mbali na kunyakuwa mara tatu taji la Bondia Bingwa wa Ngumi za Uzito wa Uzani wa Juu wa Dunia ‘World Heavyweight Champion‘, Muhammad alikuwa ndiye bondia bora wa muda wote wa dunia.
…Akiwa na David Beckham

HABARI KWA HISANI YA GPL

1 comment:

Anonymous said...

R.I.P