Advertisements

Friday, July 8, 2016

HAWA NDIO WAKURUGENZI 185 WAPYA ALIOWATANGAZA JPM



Rais John Magufuli 
RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji 5, Manispaa 21, Miji 22 na Wilaya (DC) 137 za Tanzania Bara ambao umeonesha kugusa kada tofauti za watu kutoka taasisi mbalimbali.

Uteuzi huo ulitangazwa jana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mussa Iyombe huku kati ya wakurugenzi wote 185 walioteuliwa, 65 ni wa zamani na 120 ni wapya.

Uteuzi huo unakamilisha serikali ambayo alianza kuiunda tangu Novemba mwaka jana wakati alipoteua mawaziri na manaibu wake, kisha akateua makatibu wakuu kabla ya kuteua wakuu wa mikoa Machi mwaka huu.

Aidha, baada ya uteuzi wa wakuu wa mikoa aliteua makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu tawala wa wilaya na kisha kumalizia na wakurugenzi hao aliowateua jana.

Katika uteuzi huo, mkurugenzi maarufu nchini ambaye ametumikia katika halmashauri mbalimbali nchini, Siporah Liana amekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo taarifa ya Ikulu iliyotolewa baadaye, inaonesha rais ameondoa katika orodha ya wakurugenzi hao wapya jina la Dk Leonard Masale ambaye alitajwa kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma ili kumfanya mteule huyo kuendelea kufanya kazi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, kazi aliyopangiwa hivi karibuni.

Kutokana na mabadiliko hayo, nafasi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma itabakia wazi kusubiri uteuzi utakaofanywa baadaye. Miongoni mwa taasisi ambazo wafanyakazi wake wameteuliwa ni Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha magazeti ya HabariLeo, HabariLeo Jumapili, Daily News, Sunday News na SpotiLeo.

Mhasibu katika kampuni hiyo, Shafii Mpenda ambaye pia ni Katibu wa Chama cha Wafanyakazi cha Raawu (TSN), amepangiwa halmashauri ya Madaba mkoa wa Ruvuma. Aidha, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa, Simon Berege ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari ameteuliwa kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.

Mwandishi mwandamizi mwingine aliyeteuliwa ni Mhariri wa televisheni inayomilikiwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mlimani Tv, Hamis Dambaya, anayekwenda Wilaya ya Nanyumbu. Ndani ya uteuzi huo, yumo wakili wa jijini Dar es Salaam Elias Nawela, aliyepangiwa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe.

Uteuzi mara mbili

Wakati huo huo, Ikulu imefafanua kuwa makatibu tawala wa wilaya wote ambao majina yao yamejitokeza katika orodha ya wakurugenzi wa halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na wilaya, Rais Magufuli ameamua kuwabadilishia majukumu na sasa watatumikia vyeo vyao vya ukurugenzi badala ya vyeo vya Ukatibu Tawala wa Wilaya.

Kutokana na mabadiliko hayo, nafasi za Makatibu Tawala wa Wilaya ambao wameteuliwa kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri zitajazwa baadaye. Taarifa hiyo ya Ikulu ilisema wakurugenzi wote walioteuliwa wanatakiwa kufika Ikulu Jijini Dar es Salaam, Jumanne Julai 12, saa tatu asubuhi kwa ajili ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

Orodha kamili ya wakurugenzi walioteuliwa kulingana na mikoa yao ni kama ifuatavyo;

ARUSHA

Arusha Jiji -Athumani Juma Kihamia

Arusha DC - Dk Wilson Mahera Charles

Karatu DC - Banda Kamwande Sonoko

Longido DC - Jumaa Mohamed Mhiwapijei

Meru DC - Kazeri Christopher Japhet

Monduli DC - Stephen Anderson Ulaya

Ngorongoro DC - Raphael John Siumbu

DAR ES SALAAM

Dar es Salaam Jiji - Siporah Jonathan Liana

Kinondoni Manispaa - Aron Titus Kagurumjuli

Temeke Manispaa - Nassibu Bakari Mmbaga

Ilala Manispaa - Msongela Nitu Palela

Kigamboni Manispaa - Stephen Edward Katemba

Ubungo Manispaa - Kayombo Lipesi John

DODOMA

Dodoma Manispaa - Dk Leonard M. Masale

Kondoa DC - Kibasa Falesy Mohamed

Kondoa Mji - Khalifa Kondo Mponda

Mpwapwa DC - Mohamed Ahamed Maje

Kongwa DC - Mhandisi Ngusa Laurent Izengo

Chemba DC - Semistatus Hussein Mashimba

Chamwino DC - Athuman Hamis Masasi

Bahi DC - Rachel Marcel Chuwa

GEITA

Bukombe DC - Dionis Maternus Nyinga

Chato DC - Mhandisi Joel Bahahari

Geita DC - Ally Abdallah Kidwaka

Geita Mji - Modest J. Apolinaly

Mbogwe DC - Mahwago Elias Kayandabila

Nyang’wale DC - Carlos K. Gwamagobe

IRINGA Iringa

Manispaa - William Donald Mafwele

Mafinga Mji - Saada S. Mwaruka

Mufindi DC - Riziki Salas Shemdoe

Iringa DC - Robert Mgendi Magunya

Kilolo DC - Aloyce Kwezi

KAGERA

Biharamulo DC - Wende Israel Ng’ahala

Bukoba DC - Abdulaaziz Jaad Hussein

Bukoba Manispaa - Makonda Kelvin Stephen

Karagwe DC - Godwin Moses Kitonka

Kyerwa DC - Shedrack M. Mhagama

Missenyi DC - Limbe Berbad Maurice

Muleba DC - Emmanuel Shelembi Luponya

Ngara DC - Aidan John Bahama

KATAVI

Mlele DC - Alex Revocatus Kagunze

Mpimbwe DC - Erasto Nehemia Kiwale

Mpanda DC - Ngalinda Hawamu Ahmada

Mpanda Manispaa - Michael Francis Nzyungu

Nsimbo DC - Joachim Jimmy Nchunda

KIGOMA

Buhigwe DC - Anosta Lazaro Nyamoga

Kakonko DC - Lusubilo Joel Mwakabibi

Kasulu DC - Godfrey Msongwe Masekenya

Kasulu Mji - Fatina Hussein Laay

Kigoma Ujiji - Manispaa - Judethadeus Joseph Mboya

Kigoma DC - Hanji Yusuf Godigodi

Kibondo DC - Shelembi Felician Manolo

Uvinza DC - Weja Lutobola Ng’olo

KILIMANJARO

Manispaa ya Moshi - Michael Nelson Mwandezi

Hai DC - Yohana Elia Sintoo

Siha DC - Valerian Mwargwe Juwal

Same DC - Shija Anaclaire

Mwanga DC - Golden A. Mgonzo

Rombo DC - Magreth Longino John

Moshi DC - Emalieza Sekwao Chilemeji

LINDI Kilwa DC - Bugingo I. N. Zabron

Lindi DC - Samwel Warioba Gunzar

Lindi Manispaa - Jomaary Mrisho Satura

Liwale DC - Justine Joseph Monko

Nachingwea DC - Bakari Mohamed Bakari

Ruangwa DC - Andrea Godfrey Chezue

MANYARA

Babati Mji - Fortunatus Hilario Fwema

Hanang DC - Bryceson Paul Kibasa

Mbulu DC - Festi Fungameza Fwema

Mbulu Mji - Anna Philip Mbogo

Simanjiro DC - Yefred Edson Myezi

Kiteto DC - Tamim Kambona

Babati DC - Hamis Iddi Malinga

MARA

Manispaa ya Musoma - Fidelica Gabriel Myovela

Bunda DC - Amos Jeremiah Kusaja

Bunda Mji - Janeth Peter Mayanja

Butiama DC - Solomon Kamlule Ngiliule

Musoma DC - Flora Rajab Yongolo

Serengeti DC - Juma Hamsini Seph

Rorya DC - Charles Kitanuru Chacha

Tarime DC - Apoo Castro Tindwa

Tarime Mji - Hidaya Adam Usanga

MBEYA

Busokelo DC - Eston Paul Ngilangwa

Chunya DC - Sofia Kumbuli

Kyela DC - Mussa Joseph Mgata

Mbarali DC - Kivuma Hamis Msangi

Mbeya DC - Ameichiory Biyengo Josephat

Mbeya Jiji - Zacharia Nachoa Ntandu

Rungwe DC - Loema Isaya Peter

SONGWE

Momba DC - Adrian Jovin Jungu

Tunduma Mji - Valery Alberth Kwemba

Mbozi DC - Edna Amulike Mwaigomole

Ileje DC - Haji Mussa Mnasi

Songwe DC - Elias Philemon Nawela

MOROGORO

Gairo DC - Agnes Martin Mkandya

Kilombero DC - Dennis Lazaro Londo

Ifakara Mji - Francis Kumba Ndulane

Kilosa DC - Kessy Juma Mkambala

Morogoro DC - Sudi Mussa Mpili

Morogoro Manispaa - John Kulwa Magalula

Mvomero DC - Florent Laurent Kyombo

Ulanga DC - Audax Christian Rukonge

Malinyi DC - Marcelin Rafael Ndimbwa

MTWARA

Mtwara DC - Omari Juma Kipanga

Mtwara Mikindani Manispaa - Beatrice Dominic Kwai

Masasi Mji - Gimbana Emmanuel Ntayo

Masasi DC - Mkwazu M. Changwa

Nanyumbu DC - Hamis Hassan Dambaya

Newala DC - Mussa Mohamed Chimae

Newala Mji - Andrew Frank Mgaya

Tandahimba DC - Said Ally Msomoka

Nanyamba Mji - Oscar Anatory Ng’itu

MWANZA

Mwanza Jiji - Kiomoni Kibamba Kiburwa

Ilemela Manispaa - John Paul Wanga

Kwimba DC - Pendo Anangisye Malabeja

Magu DC - Lutengano George Mwalwiba

Misungwi DC - Eliud Leonard Mwaiteleke

Ukerewe DC - Tumaini Sekwa Shija

Buchosa DC - Crispian Methew Luanda

Sengerema DC - Magesa M. Boniphace

NJOMBE

Njombe Mji - Iluminata Leonald Mwenda

Makambako Mji - Paul Sostenes Malala

Makete DC - Francis Emmanuel Namaumbo

Njombe DC - Monica Peter Kwiluhya

Ludewa DC - Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija

Wanging’ombe DC - Amina Mohamed Kiwanuka

PWANI

Bagamoyo DC - Azimina A. Mbilinyi

Chalinze DC - Edes Philip Lukoa

Kibaha DC - Tatu Seleman Kikwete

Kibaha Mji - Jenifer Christian Omolo

Kisarawe DC - Mussa L. Gama

Mafia DC - Erick Mapunda

Mkuranga DC - Mshamu Ally Munde

Kibiti DC - Alvera Kigongo Ndabagoye

Rufiji DC - Salum Rashid Salum

RUKWA

Kalambo DC - Simon Ngagani Lyamubo

Sumbawanga DC - Nyangi John Msemakweli

Sumbawanga Manispaa - Hamid Ahmed Njovu

Nkasi DC - Julius M. Kaondo

RUVUMA

Mbinga DC - Gumbo Samanditu Gumbo

Mbinga Mji - Robert Kadaso Mageni

Namtumbo DC - Christopher Michael Kilungu

Nyasa DC - Oscar Albano Mbuzi

Songea DC - Simon Michael Bulenganija

Madaba DC - Shafi Kassim Mpenda

Tunduru DC - Abdallah Hussein Mussa

Songea Manispaa - Tina Emelye Sekambo

SHINYANGA

Kishapu DC - Stephen Murimi Magoiga

Msalala DC - Berege Sales Simon

Shinyanga

DC - Mark Emmanuel Malembeka

Kahama Mji - Anderson David Msumba

Shinyanga Manispaa - Lewis Kweyemba Kalinjuna

Ushetu DC - Michael Augustino Matomola

SIMIYU

Bariadi DC - Abdallah Mohamed Malela

Bariadi Mji - Melkizedek Oscar Humbe

Itilima DC - Mariano Manyingu

Maswa DC - Fredrick Damas Sagamiko

Busega DC - Anderson Njiginya

Meatu DC - Said F. Manoza

SINGIDA

Ikungi DC - Rustika William Turuka

Iramba DC - Linno Pius Mwageni

Mkalama DC - Martin Msuha Mtanda

Manyoni DC - Charles Edward Fussi

Itigi DC - Luhende Pius Gerald

Singida DC - Rashid Mohamed Mandoa

Singida Manispaa - Kizito L. Brava

TABORA

Igunga DC - Revocatus Lubigili Kuuli

Kaliua DC - John Marco Pima

Nzega DC - Jacob James Mtalitinya

Nzega Mji - Phillimon Mwita Magesa

Sikonge DC - Simon Saulo Ngatunga

Tabora Manispaa - Bosco Addo Ndunguru

Urambo DC - Magreth Nakainga

Tabora -Uyui - Hadija Maulid Makuani

TANGA

Tanga Jiji - Daudi R. Mayeji

Korogwe DC - George John Nyaronga

Korogwe Mji - Jumanne Kiangoshauri

Muheza DC - Luiza Osmin Mlelwa

Handeni Mji - Keneth K. Haule

Handeni DC - William Methew Mafukwe

Pangani DC - Sabas Damian Chambasi

Mkinga DC - Mkumbo Emmanuel Barnabas

Bumbuli DC - Peter Isaiah Nyalali

Kilindi DC - Clemence Andagile Mwakasenda

Lushoto DC - Kazimbaya Makwega Adeladius.

HABARI LEO

No comments: