Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kulia) akisalimiana na Katibu
Mkuu wa Baraza la Kuu la Waislamu (BAKWATA), Suleman Said Lolila wakati Waziri
huyo alipokuwa anawasili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, kwa ajili ya kushiriki
Kongamano la Viongozi wa Dini lililojadili masuala ya ugaidi. (Picha
zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba akizungumza na viongozi wa dini kuhusu
masuala mbalimbali ya amani nchini katika Kongamano la Viongozi wa Dini lililofanyika
katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam. Katika hotuba yake, Waziri
Mwigulu aliwataka viongozi hao kutokuhusisha kosa lifanyalo na mtu au watu
fulani kulifananisha na dini yake, amewaomba viongozi hao watoe ushirikiano kwa
kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu nchini. Kutoka kulia ni Askofu
Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora, Paul Ruzoka, Mufti Mkuu wa Tanzania,
Abubakary Zubeiry Bin Ally na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania
(CCT), Dk Leonard Mtaita.
Sehemu
ya viongozi wa dini walihudhuria katika Kongamano la Viongozi wa Dini nchini
lililofanyika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment